HALMASHAURI ya wilaya ya Mlimba mkoani Morogoro imetoa jumla ya shilingi milioni 918 kwa ajili ya kuvikopesha vikundi 100 vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Mhandisi Stephano Kaliwa amesema fedha hizo zimetolewa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na jumla ya wanufaika 1664 watafaidika na mkopo huo.
Akizungumza katika makabidhiano ya fedha hizo sambamba na pikipiki 20 kwa wanufaika,Kaliwa amesema kwa mwaka huu wa fedha walitenga shilingi milioni 275 ikiwa ni asikimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya makundi hayo maalum.
Mhandisi Kaliwa amesema vilevile halmashauri hiyo imefanikiwa kukusanya shilingi milioni 643 ikiwa ni fedha za marejesho ya mkopo wa miaka ya nyuma hivyo kufanikiwa kupata jumla ya shilingi milioni 918 ambazo zimekopeshwa kwa walengwa hao.
Amebainisha kuwa katika fedha hizo jumla ya wanawake 1189 wamekopeshwa huku vijana ikiwa ni 467 na watu wenye ulemavu ni 8 ambapo tarafa ya Mlimba vikundi vimekopeshwa shilingi milioni 273 na tarafa ya Mngeta vimekopeshwa shilingi milionj 645
Mkurugenzi huyo mtendaji amesema wanufaika wa mkopo huo watatumia kutekeleza shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ikiwemo kilimo,ufugaji,ujasiliamali,usafirishaji na usindikaji mazao.
Naye mgeni rasmi katika makabidhiano hayo mbunge wa jimbo la Mlimba Godwin Kunambi amesema kilichofanyika ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambapo waliahidi kuwakopesha wananchi mkopo usio na riba ili kuwaletea maendeleo na kuwainua kiuchumi.
Kunambi amesema kwa kipindi cha miezi 11 toka yeye pamoja na Rais na madiwani wa chama hicho waingie madarakani mambo mengi ya maendeleo yamefanyika katika sekta mbalimbali wilayani humo.
Amesema ushirikiano baina ya madiwani na watendaji ndio umefanikisha kupatikana kwa fedha hizo ambazo ni kodi za wananchi na kuwaomba wote waliochukua mikopo kurejesha kwa wakati ili wananchi wengine nao waweze kukopeshwa.
Nao wanufaika wa mikopp hiyo wameipongeza halmashauri kwa kuwakopesha kiasi walichotaka na kusema kuwa walengwa wengi wamejipanga kutokuwa tegemezi na kusema kuwa fedha zilizotolewa mwaka huu ni nyingi na walengwa watatumiza malengo yao kwa asilimia kubwa.
Mngeta Kijiji cha Itongoa
Anuani: P.O.BOX 263
Simu: 023 293 1523
Mobile: 0232931523
Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa