• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
KILOMBERO DISTRICT COUNCIL
KILOMBERO DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa wilaya ya kilombero, akagua mipaka ya pori tengefu Kilombero.

Posted on: December 4th, 2018

Pichani juu: Mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo (Mwenye shati la kitenge la orange) akiwaonyesha wananchi kupitia ramani iliyopo kwenye simu yake, eneo la mpaka wa pori tengefu la Kilombero. 

Mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo, jana amefanya ukaguzi wa mipaka yote inayolalamikiwa ya pori Tengefu la Kilombero, ili kujiridhisha kutokana na malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Idandu, ambao wameiomba serikali iwaongezee eneo kutoka katika eneo hilo.

Wananchi hao wanadai kuwa ni eneo lao pekee, ndilo mpaka wake una eneo dogo sana ukilinganisha na vijiji vya Mofu na Kalenga, ambapo wao wanaonekana wapo kwa mbele zaidi ya kijiji cha Idandu

Hata hivyo Ndg Ihunyo aliwaeleza kuwa, Tayari watendaji kutoka katika idara ya Ardhi ya wilaya ya Kilombero, wamekwishafanya busara ya kutosha sana, kwani tayari wamewasaidia kwa kuwaongezea zaidi ya kilometa moja na nusu kutoka katika mpaka wa mkuruza wa okoa bonde na kuongeza kuwa si cha mita miatano tena mbele ili kuweza kufikisha ukubwa wa kilometa mbili, hivyo wao kama wananchi wanatakiwa kuishukuru sana serikali, hususan watendaji hao wa Ardhi kwani laiti kama angekuwa yeye asingeweza kuwa na ujasiri huo wa kuweza kuongeza hata mita mbili.

Pamoja na hayo, bado Ndg Ihunyo amesisitiza kuendelea kuwasaidia wananchi hao wa kijiji cha Idandu kwa kuwaomba waendelee kuwa watulivu kwani tayari mipaka amekwishaiona, na atapata nafasi ya kwenda kuiona mipaka mingine ya eneo linalolalamikiwa na wananchi hao la msitu wa Namwai na kuja na majibu sahihi ya namna ya kuweza kuliendea suala hilo kwa mipaka yote katika sehemu hizo mbili, siku ya Alhamisi ya tarehe 6/12/2018 kwenye majira ya saa nane mchana,atakapokutana na wananchi hao, kwenye kijiji hicho cha Idandu ili wananchi wapate kusikia kitakachoamuliwa na serikali, kwa maslahi yake na wananchi kwa ujumla.

Aidha amewataka wananchi wote ambao wanamiliki maeneo makubwa, yaliyo zaidi ya heka hamsini wayarudishe kijijini kwani hao ndio wanaosababisha upungufu wa maeneo, na wanakijiji wengine kukosa maeneo kwa kuhodhiwa na watu wachache, hali ambayo inapelekea wananchi hao kuomba maeneo mengine ambayo hayahitajiki kupewa wananchi, kama inavyotokea katika eneo hilo la kijiji cha Idandu.

‘’Tatizo kubwa linalofanya ninyi wananchi kuiona serikali haitaki kusikiliza maombi yenu juu ya kuongezewa vipande vya ardhi mnavyovitaka ni kuwa, kuna baadhi ya wenzenu wanamiliki zaidi ya heka mia tano, kitu ambacho kwa mujibu wa sheria za umilikaji ardhi vijijini, ni kinyume na sheria, kwani mwisho wa kumiliki ardhi kwa sheria za vijiji ni heka Hamsini na ikiwa itazidi hapo, ni lazima wizara ya Ardhi ihusishwe.’’ Alisema.

Ndg Ihunyo amesema kuwa, serikali ya wilaya ya Kilombero imefanya uainishaji mpya wa mipaka, ambapo vijiji zaidi ya 23 vimehusishwa, ili kuweza kuyalinda maeneo yote ambayo ni hifadhi za taifa iwe mapori au hata Ardhi tepetepe, kwaajili ya maslahi ya Taifa kwa ujumla.

Nao wananchi wamesema kuwa wamekubaliana na maagizo ya mkuu wa wilaya na kusema kuwa wamekwishaona njia ya utatuzi wa matatizo yao, pamoja na hayo wameahidi kushirikiana na serikali ya wilaya ya Kilombero, ili kuweza kuhakikisha kuwa kila mmoja anapata maeneo ya kufanyia shughuli zake za kimaendeleo.

Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOFAULU MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2019 HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO December 09, 2019
  • TAHADHARI NA UTAPELI September 21, 2018
  • FURSA KATIKA SEKTA YA KILIMO March 27, 2017
  • MAENEO YA UWEKEZAJI KWA KILIMO CHA UMWAGILIAJI March 26, 2017
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Katibu wa CCM asisitiza kutumia majina ya waasisi kwenye mashindano Kilombero

    November 09, 2019
  • Kilombero yafanikiwa kwenye chanjo

    October 25, 2019
  • Mkuu wa wilaya ya Kilombero azindua chanjo ya Surua Lubera

    October 17, 2019
  • Halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuhamia Mngeta

    October 16, 2019
  • Angalia zote

Video

MAKAO MAKUU KILOMBERODC KUHAMIA MNGETA
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Kibaoni Ifakara Morogoro

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa