• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Kilombero yapata pesa za ujenzi wa hospitali ya Halmashauri yao

Posted on: September 5th, 2019

Pichani juu: Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero ndugu David Ligazio akiwa katika kikao cha Baraza la madiwani

MADIWANI katika halmashauri ya Wilaya ya Kilombero wamewaagiza wataalamu katika halmashauri hiyo waangalie eneo gani katika Kata tatu patakapofaa kujengwa hospitali ya serikali ya halmashauri hiyo.

Agizo hilo limetolewa Jana katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo ambapo pamoja na mambo mengine pia kulifanyika uchaguzi wa makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Kata zilizopendekezwa na madiwani hao ili mojawapo paweze kujengwa hospitali hiyo ni Namwawala,Chita au Mngeta.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo David Ligazio alisema madiwani waliridhia ujenzi wa hospitali hiyo kujengwa katikati ya Wilaya ili kuondoa msongamano na umbali wa kutoka eneo moja kwenda eneo jingine.

Diwani wa kata ya Namwawala Muya Msulwa alisema wao wameshatenga maeneo kwa ajili ya ujenzi huo na wananchi wanasubiri kwa hamu ukizingatia kuwa kata hiyo ipo katikati ya Wilaya.

Lakini Diwani wa kata ya Idete Edward Kitaly alisema kuwa ujenzi wa hospitali hiyo Namwawala unaweza ukaikosesha halmashauri hospitali kwani taarifa alizonazo ni kwamba Kata ya Ifakara inaweza kuwa jimbo hivyo kata ya Namwawala kuweza kumezwa na kuingizwa halmashauri ya Mji Ifakara na kushauri hospitali hiyo kusogezwa eneo la Mngeta ama Chita.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, ndipo Mh. Ligazio aliwataarifu wajumbe wa kikao hicho kuwa wataalamu wa halmashauri wanatakiwa kuangalia mapendekezo ya madiwani na kuona wapi kutafaa ujenzi wa hospitali hiyo

Awali ilielezwa kuwa halmashauri inataraji kupata Fedha kiasi cha shilingi milioni 500 toka hazina za kuanza ujenzi wa hospitali ya halmashauri ya Wilaya na fedha hizo zinaweza kuletwa wakati wowote kutoka sasa.

Ligazio alisema mapendekezo yalielekeza hospitali ijengwe eneo la Namwawala kwani pamoja na vigezo vingine vya kisekta,vikao vya serikali za vijiji na Kata katika Kata husika vimeainisha maeneo mawili yenye zaidi ya ekari 30 kila eneo kwa ajili ya mradi huo.

Alisema maeneo yaliyopendekezwa hayakuwa na fidia kwani ni ya serikali na baada ya taarifa hiyo kuwasilishwa kamati iliridhia hospitali ya halmashauri ya Wilaya ijengwe katika jimbo la Mlimba isipokuwa wajumbe wanaotoka eneo la jimbo hilo wakubaliane eneo itakapojengwa hospitali hiyo kulingana na vigezo vilivyowekwa

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa