• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

PONGEZI KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO

Posted on: August 1st, 2017

Halmashauri ya wilaya ya Kilombero imepongezwa kwa kupata hati safi kutoka kwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG)kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.


Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Steven Kebwe katika hotuba yake iliyosomwa na ndugu, Ramadhani Kazimoto katibu tawala msaidizi serikali za mitaa morogoro aliyemwakilisha katika kikao cha baraza la madiwani wa halamashauri ya wilaya ya Kilombero kilichofanyika Julai 28,2017.


Katika hotuba hiyo Dkt Kebwe alisema halmashauri ya wilaya ya Kilombero tangu mwaka wa fedha wa 2013/14 hadi mwaka wa fedha wa 2015/16 imekuwa ikipata hati safi inayoridhisha jambo aliloeleza kwamba linastahili pongezi kwakuwa ni halmashauri chache nchini ambazo zimekuwa zikipata hati safi zinazoridhisha kwa mfululizo.


‘Mimi tangu nimefika katika mkoa wa Morogoro ,nimekuwa nikishuhudia kila mwaka mkipata hati safi inayoridhisha hivyo nawapongeza na nawaomba muendeleze hali hii na ikiwezekana mpate hati ya kiwango cha ubora zaidi ili halmashauri hiii iendelee kuwa mfano kwa halmashauri zingine katika mkoa wa Morogoro na nchi kwa ujumla’.


Aidha alitumia fursa hiyo kuishauri halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuyafanyia kazi mapendekezo  yanayotolewa na ofisi ya makaguzi mkuu wa hesabu za serikali ili iweze kufikia kiwango cha asilimia 20% ya uchangiaji wa bajeti yake ya ndani.


Kwa upande wake mdhibiti na mkaguzi wa serikali mkoa wa Mororogoro ndugu, Mwabwanga  alieleza kuwa Katika mwaka wa fedha wa 2015/16 mdhibiti na mkaguzi wa mahesabu ya serikali alifanya ukaguzi katika mamlaka za serikali za mitaa 171 ambapo ilibainika kuwa halmashauri 138 zilipata hati inayoridhisha ambapo kati ya hizo halmashauri tano zilitoka mkoani Morogoro ikiwemo  halmahauri ya wilaya Kilombero, jambo aliloeleza kuwa ni la kujivunia.


Bwana Mwabwanga aliongeza kuwa, mkoa wa Morogoro umefanikiwa katika baadhi ya Halmashauri zake kupata hati zinazoridisha ikiwemo halmashauri ya wilaya ya Kilombero ambayo ndiyo iliyoongoza ambapo pia kuanzia mwaka 2011/12 hadi 2015/16 imeendelea kupata hati inayoridhisha na pia imekuwa ikiyafanyia kazi mapendekezo ya mkaguzii mkuu wa mahesabu ya serikali nchini kwani ilikuwa na mapendekezo 52 ya kuyafanyia kazi na mapendekezo 49 kati ya hayo yametekelezwa ikiwa ni sawa na 94% ya utekelezwaji aidha kamati ya kudumu ya hesabu ya serikalii za mitaa ilitoa maagizo 10 kwa halmashauri ya wilaya ya Kilombero mwaka 2013 ambapo maagizo hayo yalitekelezwa kwa  asilimia zote na hivyo kuipongeza kwa ufanisi huo.


Aidha aliwaomba madiwani pamoja na watendaji wa serikali kushirikiana ili kuweza kufikia lengo la kukusanya bilioni 3.3 kwa kuhakikisha kwamba mifumo rasmi ya ukusanyaji wa mapato ya serikali inatumika ipasavyo, huku akitumia fursa hiyo kuelezea athari za ucheleweshwaji wa fedha za shughuli za maendeleo katika halmashauri zilizopo mkoani Morogoro.


Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero ndugu Daudi Ligazio alisema  kuwa katika mwaka wa fedha wa 2016/17, halmashauri ya wilaya ya Kilombero iliazimia kukusanya bilioni 3.6 na kufanikiwa kukusanya asilimia 92 ya fedha hizo  na kuongeza kuwa halmashauri imefanikiwa kupeleka fedha katika miradi mbalilmbali ya maendeleo ikiwemo miradi ya ujenzi wa nyumba za waalimu, vyoo, madawati pamoja na utekelezwaji wa miradi ya maji katika vijiji 14, pamoja na ukarabati wa barabara kwa kwa ufadhili wa jumuiya ya Ulaya(Barabara ya Chita - Merela) na kufafanua kuwa  jiografia ya halmashauri ya wilaya hiyo imekuwa ni changamoto kubwa inayopelekea uchelewaji wa kukamilika kwa miradi mingi kwa wakati na kuahidi kuwa wataendelea kuyafanyia kazi mapendekezo ya mkaguzi wa hesabu za serikali.


Kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika Julai, 28 mwaka 2017 ni kikao cha mwisho kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 ambapo pia pamoja na mambo mengine baraza hilo lilifanya uchaguzi wa makamu mwenyekiti wa halmashauri hiyo kwa kumchagua Bwana Emmanuel Ndangalasi (CCM),  kupitisha muhtasari wa kikao kilichopita na kushiriki katika zoezi la upimaji wa Afya wa hiari huku pia likihudhuriwa na wajumbe wote wa baraza hilo wakiwemo katibu tawala wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero aliyemuwakilisha mkuu wa wilaya hiyo wabunge wa majimbo ya Kilombero na Mlimba , viongozi wa vyama vya siasa, wadau wa maendeleo pamoja na wananchi wakazi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero.


Mwandishi ; Ibrahim Rojala



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa