• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

WIKI YA ELIMU KILOMBERO - WAZAZI WASISITIZWA KUONGEZA USHIRIKIANO NA WALIMU KUINUA TAALUMA YA WANAFUNZI

Posted on: May 11th, 2017


Katibu Tawala wilayani Kilombero Mh. Robert Selasela ametoa ushauri kwa wazazi kuongeza ushirikiano na walimu ili kuondoa uadui baina ya wazazi na walimu na badala yake wazazi kupitia umoja wa wazazi (UWAWA) wawe sehemu chanya ya kusababisha wanafunzi kujifunza ili kuimarisha elimu ya mtoto shuleni, katika kuhakikisha mwanafunzi anajifunza vyema. katibu tawala amewaomba UWAWA kuwashawishi wazazi wenzao kuchangia ili kuwawezesha wanafunzi kupata mlo wanapokuwa shuleni pia amewataka walimu pamoja na viongozi wa kisiasa katika ajenda zao za vikao kuwashawawishi wazazi umuhimu wa kupata mlo wanapokuwa shuleni ili waweze kupata elimu bora na walimu watapata fursa ya kuwawekea maarifa kwa muda wote wanapokuwa shuleni, Selasela ameyasema hayo katika maazimisho ya Wiki ya Elimu - Kilombero yaliyofanyika  Mang'ula kata ya Mwaya.

Awali katibu tawala alitembelea maonesho ya zana za kufundishia na kushuhudia walimu pamoja na wanafunzi wakitumia zana za asili na za kisasa kufundishia ambapo alitumia muda huo kuwasisitiza walimu kwamba zana hizo zisiishie kwenye maonesho tu bali pia ziendelee kutumika  darasani ili kuwaandaa vizuri wanafunzi kwa kuwajengea msingi wa elimu kwa vitendo ambapo wanafunzi mara baada ya kuhitimu masomo yao wawe ni watu bora kuitumia elimu yao kwa vitendo.


Aidha Mh. Selasela ameagiza walimu kuendeleza vipaji vya wanafunzi ambao wametengeneza zana za kufundishia ili kukuza vipaji vyao na kuhuisha dhana ya elimu ya kujitegemea ambapo vipaji vyao vitatumika kuwanufaisha katika maisha yao ya baadaye, wakati huohuo katibu tawala Kilombero amewaelekeza wataaluma na walimu wa shule za msingi kuona umuhimu wa kuwafundisha  wanafunzi masomo ya sayansi kwa vitendo (practical) ili mwanafunzi anapofika sekondari apate muendelezo wa practical kwa urahisi na ufasaha zaidi.


Akitoa hotuba yake Katibu tawala huyo amemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri kwa kushirikiana na afisa elimu sekondari kuwawezesha walimu wanaotumia teknolojia ya sayansi kuwafundisha wanafunzi  kwa kuwanunulia vifaa vya teknolojia ya habari na mawasiliano badala ya walimu hao kutumia vifaa vyao binafsi, aliyasema hayo baada ya kushuhudia ufundishaji wa mfumo wa jua linavyozunguka kwenye mhimili wake huku mzunguko huo ukiwa unaonekana kwa kutumia mashine ya projector ambapo vifaa vilivyokuwa vinatumika ni vya wenyewe walimu binafsi.


Bwana Selasela aliendelea kusisitiza kwa kuwaomba wadau wa elimu Kilombero shirika la Plan International kukisaidia kituo cha ufundi Kisawasawa ili taasisi hiyo ya ufundi iwe ni sehemu ya kimbilio la kuwasaidia vijana wa Kilombero katika kujifunza stadi za ufundi, pia amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kilombero kufanya jitihada za makusudi kukitangaza zaidi kituo hicho cha ufundi nje ya Kilombero ili mkoa mzima uweze kukifahamu na kupelekea watu wenye uhitaji wa mafunzo yanayotolewa na kituo waweze kujiunga na chuo hicho cha ufundi Kisawasawa.


Akihitimisha khotuba yake  Mh. Selasela amewataka walimu kuendelea kutimiza majukumu yao kwa kutoa maarifa kwa wanafunzi wakati serikali ikiendelea kuwajibika kutatua changamoto zao,huku  akiwataka walimu hao kuachana na visngizio vya kila siku pamoja na kuachana na siasa wakati wanapotimiliza majukumu yao shuleni. 

 





Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa