• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

STAKABADHI GHALANI INALIPA KWA MKULIMA NA HALMASHAURI

Posted on: September 10th, 2024

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Wenyeviti wa Vyama vya Ushirika vilivyomo kwenye Halmashauri ya Mlimba, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika cha UKICU, wamefanya kikao kutathmini mwenendo wa mauzo ya mazao ya Kakao na Ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ambao Halmashauri ya Wilaya Mlimba imeanza kuutumia mnamo mwezi Juni, 2024.

Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Mlimba ndg. Juma Abeleu amesema tangu Juni 12, 2024 Halmashauri  ilipoingia kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani mpaka sasa, jumla ya minada minne ya Kakao imefanyika, kilo 117,180 za Kakao zimeuzwa na kuwaingizia wakulima jumla ya shilingi 2, 205,928,200 huku Halmashauri ikiwa imepata ushuru shilingi 80,317,314 ambayo ni asilimia tatu ya mauzo ya zao husika.

Kando ya mafanikio hayo, wanakamati walitaja changamoto zinazo kabili zoezi la uuzaji wa mazao kwa njia ya stakabdhi ghalani. Miongoni mwa changamoto hizo ni baadhi ya wakulima kutoridhika na bei na kutaka kutoa mzigo yao ghalani, uhaba wa wataalamu kwenye baadhi ya vyama vya msingi, upinzani kutoka kwa wafanya biashara na madalali wa mazao.

Nyingine ni watu kutojua jinsi mfumo wa stakabadhi ghalani unavyofanya kazi na faida zake kwa wakulima, ugumu wa usafirishaji wa mazao kutoka AMCOS kwenda ghalani, ucheleweshwaji wa malipo toka AMCOS kwenda kwa wakulima, uhaba wa vifungashio na ukosefu wa benki ya Kokoa mbichi.

Hata hivyo, wana kamati hawakuishia kutaja changamoto tu bali wametoa maoni yao ya nini kifanyike kuondoakana nazo, ikiwemo kuhakikisha elimu kuhusu mfumo wa stakabadhi ghalani, manufaa ya mazao ya kimkakati, ubora wa bidhaa inapelekwa moja kwa moja kwa wakulima, kuwepo na vifungashio vyenye nembo ya Chama Kikuu cha Ushirika cha UKICU na Watendaji wa Kata na Vijiji kujengewa uwezo kuhusu zoezi zima la uuzaji wa mazao kupitia stakabadhi ghalani ili waweze kuongeza nguvu katika kuelimisha wakulima kuhusu mfumo huo.

Naye Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika cha UKICU amewataka wenyeviti wa AMCOS kutambua kwamba  sasa wanapaswa kuimarika katika vyma vyao ili walanguzi wasiwe na nguvu kuliko Vyama vya Ushirika ama wakulima.

Amesema hiyo itasaidia pindi mkulima anapokubali bei pasiwepo na kigugumizi katika kuendelea na bei hiyo, kama ambavyo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara kutokana na kwamba kwa sasa madalali na wafanyabiashara ambao wengi wao hawana nia njema na mnada, ndio wanaoleta mazao ghalani na sio mkulima.

Amewataka wenyeviti hao wawapo ghalani wakati wa mnada wazingatie zaidi wakulima na sio nani kaleta mazao ghalani.

MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa