• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

NAIBU KATIBU MKUU WA TAMISEMI ANAYESHUGHULIKIA MASUALA YA AFYA AZURU MLIMBA DC

Posted on: November 19th, 2025

Jumatatu tarehe 17.11.2025 Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI, anayeshughulikia masuala ya afya, Prof. Tumaini Nagu alifanya ziara ya kikazi kwenye Halmashauri ya Wilaya Mlimba kukagua miundombinu na huduma za afya katika Hospitali ya Halmashauri, na Zahanati ya Mbingu.

Kupitia ziara hiyo, Prof. Nagu amesema TAMISEMI itahakikisha inatatua changamoto ya uhaba wa watumishi wa afya hasa katika Hospitali ya Halmashauri, kuleta gari la wagonjwa (ambulance), na kuhakikisha stahiki za watumishi wa afya zinaendelea kulipwa kwa wakati ili kuendelea kuimarisha sekta hiyo.

Amesema ndani ya mwezi mmoja TAMISEMI itahakikisha inaanza kutatua changamoto hizo kisha akasisitiza usalama wa vifaa na vifaa tiba, pamoja na usajili wa vichanga ndani ya siku 90 baada ya kuzaliwa.

Prof. Nagu ametoa pongezi nyingi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mlimba na Menejimenti ya Sekta ya Afya kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa miundombinu ya afya, ukusanyaji wa mapato ya Hospitali, vifaa na vifaa tiba hali inayopelekea Halmashauri ya Mlimba kuwa na mazingira mazuri ya kazi kwa watumishi wa sekta ya afya.

Akiwa katika Hospitali ya Halmashauri, Prof. Nagu alikagua majengo mapya ya wodi za upasuaji, wodi za wanawake, wanaume, watoto na jengo la mama na mtoto. Mengine ni jengo la mionzi, maabara, jengo la huduma za wagonjwa wa nje na nyumba tatu kwa moja ya watumishi, iliyojengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri.

Kando ya ukaguzi wa miundombinu na utoaji wa huduma, Prof. Nagu alipokea maoni kutoka kwa wanufaika wa huduma za afya katika Hospitali ya Halmashauri wakiwemo wajawazito na wagonjwa wa nje, kisha akawahimiza kujiunga na huduma ya Bima ya Afya kwa wote akisema huduma hiyo ndio muarobaini wa upatikanaji wa matibabu wakati wote.

Kwa aupande mwingine Prof. Nagu alitembelea Zahanati ya kijiji cha Mbingu ambapo pia alipongeza utoaji wa huduma kwa wananchi.

Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI katika Halmashauri ya Wilaya Mlimba imekuwa chachu kwa watumishi wa sekta ya afya na halmashauri kwa ujumla na hii imedhihirika katika maneno ya ufunguzi wa hotuba yake kwa watumishi wa sekta ya afya, na timu ya menejimenti ya halmashauri ambapo alisema,

“sisi tumekuja kuangalia huduma za afya, kuangalia mazingira yenu, kuwatia moyo na kuonja changamoto mnazozipitia katika uhalisia wake na kwa kweli tumefurahishwa sana na utendaji wenu. Kwa kweli mnastahili pongezi kubwa sana”.

Prof. Nagu katika ziara hiyo aliambatana na wataalamu kutoka wizarani kwake, mkoani, MSD, Bima ya Afya kwa Wote.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU 2025 July 03, 2025
  • TANGAZO LA KUTEULIWA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO WASIMAMIZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NAIBU KATIBU MKUU WA TAMISEMI ANAYESHUGHULIKIA MASUALA YA AFYA AZURU MLIMBA DC

    November 19, 2025
  • MWANZO WA SAFARI YA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA KATI YA SERIKALI YA MAPINDUZI YANZANZIBAR NA HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA

    October 23, 2025
  • TAARIFA YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WALOFANYA MTIHANI WA TAIFA 2025 MLIMBA DC

    October 23, 2025
  • MKURUGENZI MLIMBADC AFANYA MAZUNGUMZO NA TIMU YA MKOA YA USIMAMIZI WA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

    October 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa