• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • mazingira yetu
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • FOLUR
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MKURUGENZI MLIMBADC AFANYA MAZUNGUMZO NA TIMU YA MKOA YA USIMAMIZI WA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

Posted on: October 17th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, Ndg. Jamary Idrisa Abdul amefanya mazungumzo na Timu ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala Ngazi ya Mkoa baada ya kuwapokea Ofisini kwake leo asubuhi tarehe 17.10.2025.

Mkurugenzi Mtendaji ameishukuru timu hiyo kwa kusaidia kuasisi mauzo ya mazao ya biashara kwa mfumo wa stakabadhi za ghala ndani ya Halmashauri ya Mlimba ambapo mpaka sasa mazao manne; kakao, korosho, ufuta na mbaazi yanauzwa kwa njia hiyo, wakulima na halmashauri wananufaika.

Mbali na changamoto ikiwemo ya miundombinu ya barabara hasa wakati wa masika, Mkurugenzi Jamary ameiomba timu ya usimamizi wa mfumo wa stakabadhi za ghala ngazi ya mkoa kuliingiza shamba la korosho la halmashauri katika ushindani wa wazalishaji wakubwa unaoratibiwa na Bodi ya zao hilo nchini ili halmashauri iweze kunufaika zaidi kupitia zao hilo.

Kwa upande wake Mrajis Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Morogoro, Ndg. Cesilia Sostenes amempongeza Mkurugenzi na wataalamu wake kwa usimamizi mzuri wa vyama vya ushirika unaobainika kupitia utulivu wa vyama hivyo kwani hakuna changamoto za malipo na wakulima wanaendela kuonesha imani kwa vyama vyao kwa kuendelea kukusanya na kuuza mazao yao kupitia vyama hivyo.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mali, Dkt. Rosalia Rwegasira naye amempongeza Mkurugenzi na wataalamu wake kwa kufanya kazi kama timu na kuwaagiza wasimamie suala la ubora wa mbegu kwa wakulima ili kuweza kuongeza uzalishaji na kuimarisha zaidi uchumi wakulima na wananchi wa Mlimba kwa ujumla.

Pamoja na ahadi ya kushughulikia changamoto zilizo wasilishwa kikaoni hapo, ikiwemo ya miundombinu ya barabara na mabadiliko ya bei za mazao, kiongozi wa msafara huo ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Ndg. Beatrice Njawa amemtaka mkurugenzi kuwekeza katika ujenzi wa maghala ya mazao mchanganyiko katika kata zake ili kutatua changamoto ya uhaba wa huduma hiyo ndani ya halmashauri.


Pia ameitaka halmashauri kuanza kufikiria kupunguza kuuza mazao ghafi kwa kuyaongezea thamani huku akihimiza uongezaji ubora wa zao la kakao kwa kuzikausha kwa makaushio ya kisasa.

Timu ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala Mkoa wa Morogoro imeendelea  kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa mfumo ndani ya halmashauri zake zenye kuzalisha mazao ya kimkakati ikiwemo Halmashauri ya Mji Ifakara, Halmashauri ya Wilaya Mvomero, Malinyi na Ulanga ili kujua changamoto na mafanikio yaliyokwisha kupatikana.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA YAPOKEA WAAJIRIWA 118

    January 20, 2026
  • HALMASHAURI YA MLIMBA YAKEMEA UCHIMBAJI HOLELA WA VIFUSI NA UHARIBIFU WA MTO MNGETA, YAAHIDI KUDHIBITI NYANI WAHARIBIFU KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA KIBURUBUTU

    January 19, 2026
  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa