• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Wana Kilombero waaswa kushirikiana kulinusuru bonde la Kilombero

Posted on: March 9th, 2019

Pichani juu: Naibu waziri wa nchi ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe. Musa Sima (aliyesimama) akizungumza na viongozi wa wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi.

Viongozi katika Bonde la Kilombero wamehimizwa wawe na ushirikiano  katika utendaji Wa kazi zao ili kulinusuru Bonde hilo.

Wito huo umetolewa  na  Naibu Waziri Wa nchi,Ofisi ya Makamu Wa Rais Muungano na Mazingira Musa Sima wakati akizungumza na viongozi Wa Wilaya za Kilombero,Ulanga na Malinyi katika mkutano uliofanyika  mjini Ifakara.

Sima amesema kama watendaji na viongozi Wa kuchaguliwa wakifanya kazi kwa pamoja na baadae kutoa elimu kwa wananchi ana imani hakutakuwa na migogoro katika Bonde hilo ambalo ndio tegemeo la Maji katika mto Rufiji.

Amesema kama kila kiongozi akifanya kazi kwa matakwa yake basi migogoro na uharibifu wa bonde hilo utaendelea kuwepo sababu hakutakuwa na kiunganishi baina ya wananchi na serikali.

Naibu waziri aliyasema hayo baada ya awali kuwasikiliza  wakuu Wa Wilaya hizo na wenyeviti Wa halmashauri kuelezea hali halisi ya Bonde la Kilombero ambapo kila upande ulimlaumu mwenzake kuwa kwa namna moja ama nyingine unachangia uharibifu huo.

Wakuu Wa Wilaya walisema kuwa juhudi kubwa zinafanywa kwa ushirikiano Wa wakuu Wa Wilaya zote tatu ila inapofikia katika utekelezaji Wa maagizo wanasiasa uwakingia kifua wananchi na hali hiyo usababisha mambo kuharibika.

Kwa upande wao wenyeviti Wa halmashauri walisema kuwa tatizo lipo kwa baadhi ya watendaji ambao utoa maagizo ya ghafla kwa wananchi bila kuwaandaa na kudai kuwa hakuna anaepinga uhifadhi Wa Bonde hilo ila taarifa zinatakiwa kutolewa kwa wakati.

Naibu waziri alisema inaonyesha kuwa hakuna ushirikiano Wa karibu katika kulilinda Bonde hilo hivyo kuwataka viongozi kuwa na ushirikiano Wa pamoja kabla na baada ya kufanya maamuzi kisha kuwapa elimu wananchi na hiyo haitasababisha migongano.

Ametolea mfano kuwa Rais Magufuli anaaminiwa na wananchi wote Wa chini kwa sababu anawasikia hivyo kwa nini viongozi Wa chini hawaaminiwi na wananchi?,alihoji.

Kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa kijiji cha Ngombo baada ya mawaziri 8 kutembelea eneo hilo hivi karibuni ,Sima aliwataka viongozi wa Wilaya hizo wawe na subira kwani hivi karibuni watampatia maelekezo na ushauri Rais na yeye kutoa majibu.

Alisema toka walipofika katika kijiji hicho na maeneo mengine timu ya mawaziri 8 wamegundua mapungufu kadhaa ikiwemo maeneo mengine kuwa chepechepe huku maeneo mengine yakionekana vitongoji ndio vimeingia katika hifadhi na sio kijiji kizima

Hata hivyo naibu waziri huyo amewataka watendaji wawe na utu na sio kung'ang'ania tu Sheria wanapotaka kuwatoa wananchi kwani iwananchi wanapenda hifadhi ila binadamu nao wana thamani yao.
Ametoa maagizo kwa wataalamu Wa mazingira kupeleka kwa wakuu Wa Wilaya mpango kazi Wa uhifadhi Wa ikolojia na uhifadhi Wa mazingira na kuwepo na kamati za mazingira kuanzia ngazi ya chini na ziwe kamati hai.

Awali wakuu Wa Wilaya hizo walimweleza naibu waziri kuwa wana ushirikiano Wa pamoja katika kulitunza bonde la Kilombero na sasa wanasuburi kauli ya serikali kuhusu kijiji cha Ngombo kutokana na hivi sasa kuwepo na mapigano baina ya wakulima na Wafugaji kugombea kijiji hicho.

Kwa upande wao wakurugenzi na wenyeviti Wa halmashauri na mhifadhi pori tengefu la Kilombero walisema changamoto kubwa inayolikabili Bonde hilo kwa sasa ni uvamizi Mkubwa Wa mifugo .

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa