• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

453 WATIBIWA NA MADAKTARI BINGWA WA MAMA SAMIA-MLIMBA

Posted on: June 8th, 2024

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Jumla ya wananchi 453 wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba wakiwemo wazee, wajawazito na watoto wamenufaika na huduma za matibabu za madaktari bingwa wa mama Samia waliokuwepo kwenye Hospitali ya Halmashauri hiyo kwa muda wa siku tano kuanzia Juni 3 hadi 7, wakitoa huduma za magonjwa ya ndani, wanawake, watoto, mifupa, upasuaji na ganzi na usingizi.

Hayo yameelezwa na Mganga Mkuu wa Wilaya Mlimba Daktari Christina Guveti, ambaye pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utekelezaji wa utoaji wa huduma hizo kwenye Hospitali 184 za Halmashauri mbalimbali kote nchini.

Aidha, Dkt. Guveti amesema yeye pamoja na wasaidizi wake wameona bado kuna uhitaji wa huduma za kibingwa kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, hivyo wanapanga kuweka namna nzuri ya kuhakikisha huduma hizo zitakuwa endelevu Hospitalini hapo.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Halmashauri Dkt. Willy ameishukuru timu ya madaktari bingwa kwa kuzindua huduma za upasuaji hospitalini hapo.

Kwa upande wao wananchi ambao ni miongoni mwa walionufaika wa huduma hizo za kibingwa hospitalini Mlimba wamesema, wameridhishwa na huduma zilizokuwa zikitolewa na madaktari bingwa na wameipongeza Serikali kwa kuona haja ya kuwasogezea wananchi huduma za kinbingwa za matibabu kupitia Hospitali za Halmashauri.

Baadhi yao wamesema ujio wa madaktari hao umekuwa suluhu kwa matatizo ya kiafya waliyodumu nayo kwa miaka mingi bila kujua undani wake.

“Nimesumbuliwa na tatizo la kuvimba miguu kwa kipindi cha zaidi ya miaka 14 lakini kupitia vipimo nilivyoandikiwa na madaktari hao, tatizo limeweza kugundulika na nimepatiwa dawa ambazo ninaamini zitaponesha kabisa tatizo nililo nalo” alieleza mmoja wa wananchi waliohudhuria hospitalini Mlimba.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba ndugu Jamary Idrisa amewapongeza na kuwashukuru madaktari hao kwa huduma nzuri walizotoa kwa wananchi kwani kupitia hizo wananchi wameweza kuona namna Serikali inavyojali afya za wananchi wake.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa