• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

BARABARA YA KIDATU - IFAKARA KUJENGWA KWA KIWANGO CHA RAMI

Posted on: August 5th, 2017

Naibu waziri ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (Tamisemi) Mh. Seleman Jaffo ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero pamoja na watumishi wa Halmashauri ya mji wa Ifakara katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya Kilombero mjini Ifakara.


Mh. Jaffo amesema Barabara ya Kidatu - Ifakara ujenzi wake uko mbioni kuanza wakati wowote kutoka hivi sasa kwa kiwango cha Rami kwa ufadhili wa umoja wa jumuiya za nchi za ulaya (european union) teyali fedha zimeshapatikana na mkataba umeshasainiwa na katibu mkuu kutoka wizara ya fedha ikiwa ni kazi kubwa iliyofanywa na Mh.  rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli.


Aidha naibu waziri amefafanua kuwa lengo ni kuwafanya watumishi pamoja na wananchi kwa ujumla kufanya kazi zao kwa amani ikiwa ni pamoja na kurahisisha usafirishaji wa mazao ya wakulima kwa urahisi zaidi  baada ya kukamilika kwa barabara.


Ziara ya Mh naibu waziri ilikuwa na lengo la kukagua miradi ya maendeleo na kuongea na watumishi ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na kupeana maelekezo ya kazi kwa watumishi wa serikali za mitaa.


Katika khotuba yake naibu waziri amewaeleza watumishi wa Kilombero kuwa dhana ya mabadiliko lazima watendaji wa serikali wabadilike katika utendaji wao wa kazi ambapo amewataka watumishi katika halmashauri zote mbili kila mtumishi ni lazima atimilize wajibu wake ili kuwatumikia wananchi.


Wakati huohuo Mh. jaffo amewasisitiza watumishi hususan wakuu wa idara kupangiana malengo kwa kujaza fomu za upimaji malengo ya kazi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 huku akihitaji kupata nakala ya fomu za wakuu wa idara wa nne kutoka idara ya maji , afya, kilimo na idara ya ujenzi ili aweze kuona malengo waliyokubalina kuyafanya kwa mwaka wa fedha 2017/2018 pia Mh. naibu waziri amehitaji nakala ya watendaji kata wanne ambao wameshafanyiwa upimaji wa tathmini zao kutoka katika kata.


Akihitimisha khotuba yake Mh. Jaffo amemtaka mkuu wa idara ya maji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero kumpatia taarifa ya miradi ya maji inayotekelezwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Kilombero pamoja na changamoto zinazoikabili miradi hiyo ifikapo jumatano ya tarehe 09/08/2017 ikiwa inaonyesha kama wakandarasi wako katika eneo la kazi ama hawako na lini miradi hiyo itakamilika. Mh waziri pia amewapongeza watumishi wa wilaya ya Kilombero kwa kufanya kazi kwa ushirikiano kati ya wakuu wa idara, watumishi, mkurugenzi pamoja na mkuu wa wilaya huku akilinganisha tofauti aliyoiona katika maeneo mengine aliyoyatembelea ndani ya halmashauri zilizopo mkoani Morogoro.








Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa