• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Chifu Ihunyo atoa tamko juu ya migogoro ya wakulima na wafugaji Kilombero.

Posted on: August 15th, 2019

Pichani juu: mkuu wa wilaya ya Kilombero Chifu James Ihunyo (katikati) akizungumza na wakulima na wafugaji (Hawapo pichani) wakizungumzia kuhusu migogoro inayoendelea wilayani humo, pembeni yake niviongozi wengine.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Chifu James Ihunyo, amewataka wafugaji wote waliokuwa ndani ya Halmashauri hiyo, kuweka alama mifugo yao yote ili iweze kujulikana, kwa lengo la kutatua baadhi ya migogoro inayoendelea kuwepo baina ya wakulima na wafugaji.

Chifu Ihunyo ameyasema hayo leo, katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Kilombero, ili kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji, baada ya kuona ongezeko la mifugo mingi isiyotambulika, ambayo mwisho wa siku huishia kwenye migogoro mikubwa sana baina ya wakulima na wafugaji.

“Baada ya kikao hiki nawaomba wafugaji wote wajiandae,kwani mifugo isiyowekwa alama hatuitaki, maana matatizo ya migogoro yanazidi kuwa mengi na hii ni kutokana na malalamiko kuwa mengi sana, kutokana na ukweli kuwa kumekuwa na ongezeko la uvamizi wa wafugaji kutoka maeneo mengine kuhamia katika wilaya hii, kitendo kinachopelekea maeneo ya malisho kuwa machache hivyo kuingilia maeneo ya wakulima ambapo hapo, migogoro ndipo inapoanzia,”amesema chifu Ihunyo.

Naye katibu wa wilaya wa chama cha wananchi CUF ndg Bashiri Ally, amesema kwa upande wake ameona wafugaji ndio wanasumbua kwa kiasi kikubwa, kwani mazao ya wakulima yamekuwa yakiharibiwa na wafugaji, hivyo kupelekea hasara kwa wakulima wa mazao hayo.

Kwa upande wake Afisa ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero Abel Mbata, amesema kuwa, wanafanya jitihada kubwa za kuweka vibao kwa ajili ya mipaka, lakini matatizo yanaanzia vijijini kwani maeneo yanayotengwa hayatoshelezi kutokana kuongezeka kwa mifugo.

Aidha akielezea kwa mifano Afisa ardhi huyo amesema, katika kijiji cha Melela kuna ng’ombe elfu tatu, kwenye eneo la hekta Alfu mbili, ambayo ina sehemu ya malisho yenye hekta mia tatu, na kwa upande wa kijiji cha Msita kina jumla ya ng’ombe elfu saba, ambapo eneo lililopo ni hekta elfu tatu, yenye sehemu ya marisho hekta mia nne.

Katika hatua nyingine Diwani wa Signal Shema Ndama amesema, kamati za kulinda maeneo ziliundwa, lakini ziliingiliwa na viongozi wa Kijiji, hivyo katika kutoa rai yake, Mh. Shema amesema kuwa, anashauri wafugaji waachiwe walinde wenyewe maeneo yao ya malisho na wawe na mamlaka nayo, hivyo mamlaka kitendo ambacho kitatoa fursa kwa wao kama wamiliki wa eneo hilo kutotoa mwanya kwa wafugaji wengine kuhamia hapo kwani kitapunguza eneo la malisho yao.

Hata hivyo kwa upande wake Afisa mifugo na uvuvi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero Dr Aneth Kitambi amesema kuwa, hatua za ukaguzi wa mifugo na utoaji wa chanjo za homa ya mapafu kwa Wanyama, zimeanza kuchukuliwa kwani wameanza Signal na Kiberege, zoezi hilo litaendelea kwenye kata zote za Halmashauri ya wilaya ya Kilombero, huku akisema kuwa uzinduzi rasmi wa zoezi hili kwa kata zote, utafanyika Tarehe 19/8/2019 katika kata ya Signal.

Sanjari na hayo Dr. Kitambi ameongeza kuwa, idadi ya wanyama kwa kila mfugaji ipo, hivyo kila mtu ataangaliwa idadi ya mifugo yake, kwa kuwa kila mfugaji ana kadi yake ya utambuzi wa Wanyama anaomiliki, hivyo mfugaji atakayebainika kuwa na mifugo migi kupita kiwango, atapewa angalau miezi sita kupunguza nifugo hiyo, na kwa wale ambao hawana kabisa kadi ya utambuzi wa Wanyama anaowamiliki, huyo atahesabika kama mvamizi wa eneo hilo na kuchukuliwa hatua ikiwamo kufukuzwa kabisa katika

eneo hilo.

Habari picha: namna kikao hicho kilivyokuwa kinaendeshwa.








Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa