• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Chifu James Ihunyo anogesha shughuli za mwenge Kilombero.

Posted on: August 6th, 2019

Pichani juu: Mkuu wa wilaya ya Kilombero Chief James Ihunyo akitoa zawadi za pesa taslimu kwa baadhi ya wananchi waliozidisha Hamasa katika mradi wa mabweni ya shule ya Upili ya Sanje

Mkuu wa wilaya ya Kilombero Chifu James Ihunyo, amesema kuwa amefurahishwa na watu waliojitoa kwa mioyo yao yote, katika kusherehesha shughuri ya Mwenge wa Uhuru, kwa lengo la kufanya muonekano mzima wa wa shughuli hiyo ifane na kupendeza.

Aidha ili kuidhihirisha furaha yake Mkuu wa Wilaya hiyo, aliamua kutoa zawadi za pesa taslim kwa baadhi ya wananchi ambao, walionekana kunogesha shughuli zaidi, kwani kwa kufanya hivyo kulipelekea kuamsha baadhi ya watu waliokaa kimya kuungana na washereheshaji wengine kwa lengo la kuchangamsha shughuli hiyo.

Katika mazungumzo yake, Chifu Ihunyo alisema kuwa kilichopelekea yeye kutoa pesa nyingi kwa wananchi katika kusherehekea mwenge wa uhuru uliopita katika Halmashauri ya wilaya ya Kilombero tarehe 05/08/2019, ni kutokana na watu kuhamasishwa vya kutosha na kupelekea shughuli hiyo kuwa ya kipekee miongoni mwa Halmashauri zote katika mkoa wa Morogoro.

Awali ilionekana kuwa mkuu huyo wa wilaya alikuwa akishiriki kucheza na wananchi waliojitokeza na kutoa shamra shamra huku akitoa zawadi mbali mbali zikiwamo pesa taslim kwa wananchi waliojijitokeza kitendo kilichopelekea wananchi hao kujitokeza kwa wingi hata kwenye mashindano kadhaa yaliyoandaliwa na mkuu huyo.

Katika Hatua nyingine Mkimbiza mwenge wa kitaifa ndugu Mzee Mkongea Ally, akiwaaga wananchi waliojitokeza katika mkesha huo katika eneo la kiberege katika halmashauri ya wilaya ya Kilombero, amesifu namna hamasa ilivyofanyika na kupelekea watu kubaki wengi kwenye mkesha ambapo watu hao wangeweza kulala majumbani kwao lakini kwa uzalendo tu wa taifa lao na mwenge kwa ujumla, wameweza kukesha na mwenge.

''Niwashukuru sana wananchi ambao mmeacha usingizi wenu na kuja kusherehekea na sisi kwenye mkesha huu wa mwenge kwa mwaka huu, kwa kweli tumefarijika sana, kwani hamasa iliyofanyika ni kubwa sana, najua mngeweza kulala majumbani mwenu lakini mmeonesha ushirikiano na uzalendo mkubwa sana mungu awabariki sana na kwaherini.'' Alimaliza.



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA YAPOKEA WAAJIRIWA 118

    January 20, 2026
  • HALMASHAURI YA MLIMBA YAKEMEA UCHIMBAJI HOLELA WA VIFUSI NA UHARIBIFU WA MTO MNGETA, YAAHIDI KUDHIBITI NYANI WAHARIBIFU KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA KIBURUBUTU

    January 19, 2026
  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa