• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA UTAWALA IMEKAGUA MIRADI 12 YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA

Posted on: January 11th, 2026


Tarehe 9 na 10 Januari 2026, Kamati ya kudumu ya Fedha, Uongozi na Utawala, ya Halmashauri ya Wilaya Mlimba imefanya ukaguzi wa miradi 12 ya maendeleo ya sekta za elimu na afya, katika kata za Masagati, Utengule, Kamwene, Mlimba, Mngeta, Igima, Namwawala na Idete, iliyotekelezwa katika kipindi cha Robo ya Pili ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 (Oktoba-Desemba).


Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Masagati, Utengule na Namwawala, pamoja na jengo la utawala, bwalo, na bweni moja katika shule ya sekondari ya wasichana ya Miembeni.

Aidha, Kamati ilikagua ujenzi wa bweni moja katika shule ya sekondari ya Matundu Hill, ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi katika kijiji cha Ngajengwa, pamoja na ujenzi wa nyumba 15 za watumishi katika kitongoji cha Itongowa B.

Pia, ilikagua ujenzi wa wodi mbili za upasuaji na nyumba tatu za watumishi wa afya katika Hospitali ya Halmashauri, mradi ambao utafanya kazi ya utoaji wa huduma za afya kuwa bora zaidi.

Kamati imepongeza kasi na ubora wa utekelezaji wa miradi hiyo, ikisema kuwa utekelezaji huo unaonesha dhamira njema ya halmashauri kusogeza huduma za msingi karibu na wananchi wake.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, Mhe. Martha Mkula, ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa kamati hiyo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuiletea halmashauri fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amefafanua kuwa miundombinu ya kisasa katika shule na vituo vya kutolea huduma za afya, pamoja na vifaa tiba vilivyopo, vinachangia kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi.

Pia kupitia ziara hiyo, Mhe. Mkula ameagiza watendaji wa kata zote kuanzisha “benki za matofali” kwa ajili ya kuongeza upatikanaji wa matofali wakati wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu, wa Halmashauri ya Mlimba, Ndg. Filbert Mbwilo, akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wakati wa ziara hiyo, amesisitiza kwamba miradi yote iliyopangwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, inatarajiwa kukamilika kwa wakati na kuanza kutumika.

Ziara ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Utawala imefanyika kwa mafanikio makubwa, ikiwa ndio ziara ya kwanza tangu kuundwa kwa kamati hiyo mwezi Desemba 2025 baada ya kiapo cha udiwani, na inaonesha matumaini ya ushirikiano bora kati ya waheshimiwa madiwani na menejimenti ya Halmshauri.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA UTAWALA IMEKAGUA MIRADI 12 YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA

    January 11, 2026
  • NAIBU KATIBU MKUU WA TAMISEMI ANAYESHUGHULIKIA MASUALA YA AFYA AZURU MLIMBA DC

    November 19, 2025
  • MWANZO WA SAFARI YA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA KATI YA SERIKALI YA MAPINDUZI YANZANZIBAR NA HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA

    October 23, 2025
  • TAARIFA YA WANAFUNZI WA DARASA LA NNE WALOFANYA MTIHANI WA TAIFA 2025 MLIMBA DC

    October 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa

  • HUSKYSLOT
  • ROBOSLOT
  • TAHUPLAY
  • AWPSLOT
  • DANATOTO