• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

DC KILOMBERO AFANYA ZOEZI LA KUSHTUKIZA NA KUKAMATA NG'OMBE 100 KILOMBERO

Posted on: August 5th, 2018

MKUU Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo sambamba na kamati yake ya ulinzi na Usalama wakishirikiana Mamlaka ya Usimamizi Wa Wanyamapori(TAWA)wamefanya zoezi la kushtukiza na kukamata ng'ombe zaidi ya 100 waliovamia hifadhi na maeneo ya wakulima.

Zoezi hilo la aina yake lilifanyika Jana katika kata ya Mofu na Dc  huyo hakutaka kuwajulisha mapema viongozi Wa kata hiyo kwa kuhofia kuvujisha siri kwa wafugaji hatimae kutorosha Mifugo yao.

Baada ya kuingia Mofu yaligawanya makundi matatu tayari kusaka Mifugo iliyoingia kinyemela na ile inayolishwa katika Mashamba ya wakulima na hatimae kundi lililoongozwa na Mkuu huyo Wa Wilaya lilifanikiwa kukamata ng'ombe zaidi ya 50.

Hata hivyo zoezi hilo halikufanikiwa kukamata ng'ombe wengi tokana na kuchelewa kufika katika kata hiyo na hiyo ilipelekea baada ya kuonekana tu wafugaji walianza kuwasiliana kwa simu na hatimae makundi makubwa ya ng'ombe kukimbizwa ama kufichwa msituni.

Ihunyo amesema ameamua kufanya zoezi la kushtukiza baada ya kupewa taarifa na raia wema kuwa hivi sasa katika kata hiyo ya Mofu kuna Mifugo mingi imeingia kutoka Wilaya Jirani ya Malinyi na kwa sasa wanachungia katika Mashamba ya wakulima na kufanya wakulima hao kushindwa kulima mahindi baada ya kivuna mpunga.

Mkuu huyo Wa Wilaya alisema toka mwaka 2012 katika kata nzima walitenga maeneo ya wakulima na wafugaji lakini anashangaa bado baadhi ya wafugaji wabishi na wanaendelea kuingiza Mifugo na kulishia katika Mashamba ya wakulima na hiyo inahatarisha kuleta migogoro ya wakulima na wafugaji.

Alisema ng'ombe wanaotakiwa katika Wilaya hiyo ni wale waliosajiliwa na kwa sasa Mifugo yote iliyokamatwa itapigwa faini ila kuna zoezi jipya litafanyika hivi karibuni na Mifugo yote itakayokamatwa wahusika watafikishwa mahakamani na Mifugo kupigwa mnada.

Amewataka wafugaji wote wilayani humo kuheshimu sheria za kuwa na Mifugo michache inayotambulika na kutoingiza Mifugo mingine ili kulinda Bonde la MTO Kilombero ambalo linatazamwa na taifa kama tegemeo la mradi Mkubwa Wa uzalishaji umeme katika mto Rufiji(Stigles gorge).

Akizungumzia kuhusu wakulima na wafugaji kutumia eneo la Bonde oevu,Ihunyo alisema msimu Wa Kilimo umeisha na yakishatolewa mazao wakulima na wafugaji hawatakiwi kuonekana tena katika maeneo hayo.

Kwa upande wake Meneja Wa poritengefu la Kilombero Linus Chuwa alisema kumekuwa na tatizo la muda mrefu la uvamizi Wa eneo hilo na wameanzisha zoezi la kuwaondoa wavamizi katika Wilaya ya Malinyi na sasa Kilombero na kutakuwa na doria endelevu lengo ni kuondoa Mifugo yote katika Bonde hilo.

Nae mmoja Wa wafugaji aliyekamatwa na Mifugo yake Chimagale Mtema alisema wanaheshimu maamuzi ya serikali ila alioeleka Mifugo yake katika Mashamba ya wakulima baada ya kuona wakulima wametoa mazao yao ila ameiomba serikali kuwatengea maeneo ya kulishia na kunyweshea Mifugo yao na hii itasaidia kutoingia maeneo ya wakulima.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa