• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

UZINDUZI WA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 MLIMBA, WAFANA

Posted on: January 7th, 2025

Na, Milka Kaswamila-Mlimba DC

Uzinduzi wa zoezi la utoaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi vwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kwa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, umefanyika jana tarehe 06.01.2024 kwa kishindo, huku Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, mhe. Wakili Dunstan Kyobya, akionesha uongozi bora kwa kukabidhi hundi ya mfano ya shilingi bilioni 2.2 na pikipiki 74 kwa vikundi vya walengwa wa mikopo hiyo.

Mkuu wa Wilaya, mhe. Dunstan Kyobya alikabidhi vitu hivyo akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba, mhe. Innocent Mwangasa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilombero huku akisisitiza umuhimu wa mikopo hiyo katika kusaidia kukuza maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika Halmashauri na Wilaya kwa ujumla.

Awali, kabla ya kukabidhi hundi hiyo ya mfano pamoja na pikipiki, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mlimba, ndg. Jamary Idrisa Abdul alifafanua kuhusu mwenendo wa utoaji wa mikopo hiyo tangu mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri hiyo ilipoanzishwa rasmi.

Mkurugenzi Jamary alisema licha ya changamoto ya baadhi ya vikundi kutorejesha kwa wakati ama kukwepa kabisa kurejesha mikopo wanayo chukua, vikundi vingi vimekuwa vikirejesha, na Halmashauri imekuwa ikiendelea kutoa mikopo kwa vikundi vya walengwa wa mikopo hiyo ambapo mwaka wa fedha 2019/2020 shilingi 400,000,000.00 zilikopeshwa na shilingi milioni 398,145,000.00 zilirejeshwa, mwaka 2020/2021 shilingi 950,670,000.00 zilikopeshwa na shilingi 950,167,000.00 zilirejeshwa.

Mwaka 2021/2022 shilingi 1,504,940,000.00 zilikopeshwa na shilingi 1,447,834,500.00 zilirejeshwa na mwaka wa fedha 2022/2023, shilingi 699,190,853.11 zilikopeshwa na shilingi 649,468,853.11 zilirejeshwa, na mwaka huu 2024/2025, Halmashauri imetenga shilingi 2,206,066,461.00 kwa ajili ya mikopo hiyo ambapo katika uzinduzi huo, jumla ya shilingi 746,795,000.00 zimeingizwa kwenye akaunti za vikundi 26 vya wanawake, 19 vya vijana na 4 vya walemavu.

Vikundi vya wanawake vimekopeshwa shilingi 388,000,000.00, vijana shilingi 330,795,000.00 na walemavu shilingi 28,000,000.00.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri, ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Jumuia za Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Morogoro, mhe. Innocent Mwangasa amevitaka vikundi vya walengwa wa mikopo hiyo kuhakikisha wanazingatia kaulimbiu ya utoaji wa mikopo hiyo “Rejesha kwa Wakati Nami Nikope” ili kutoa fursa kwa wananchi wengine wenye uhitaji wa mikopo, kuendelea kukopa na wao wenyewe kuendelea kuwa na sifa ya kukopesheka kwa awamu zingine mbeleni endapo watakuwa na uhitaji tena.

Nao wanufaika wa mikopo hiyo wamepaza sauti zao kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kibali mikopo hiyo itolewe katika Halmashauri zote nchini, ikiwemo Halmashauri ya Mlimba na wameahidi kuhakikisha wanarejesha kwa wakati ili wasiwanyime wengine fursa na kurudisha nyuma jitihada za Halmashauri na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, za kuwakwamua kiuchumi wananchi wake.

MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    February 28, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI WA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA-MLIMBA

    February 08, 2025
  • MLIMBA YAPOKEA MRADI WA MIAKA 5 WA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    February 07, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa