• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

DC KYOBYA AKAGUA MRADI WA SHULE MPYA KATIKA KATA YA IGIMA

Posted on: January 7th, 2025

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, mhe. Wakili Dunstan Kyobya, jana taerehe 06.01.2025, amekagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya Sekondari unaotekelezwa katika kijiji cha Namalumbo, Kata ya Igima kwa fedha kutoka Serikali Kuu, shilingi milioni 528.

Mhe. Kyobya, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Mlimba fedha hizo na amependekeza kwa Kata ya Igima, kupitia kwa Diwani wao kwamba ikiwa wataona vyema, shule hiyo iitwe Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia, mhe. Kyobya amewapongeza mafundi wanaotekeleza ujenzi huo kwa kufanya kazi kwa kasi na kwa ubora kwani ujenzi wa shule hiyo ulianza mwanzoni mwa mwezi Novemba, 2024 na hivi sasa ujenzi upo katika hatua ya ukamilishaji.

Majengo yanayo jengwa katika mradi huo ni vyumba nane vya madarasa, jengo la utawala, maabara tatu za sayansi, maabara moja ya Jografia, maktaba moja, jengo la TEHAMA, na vyoo matundu 8.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Wilaya amempongeza Mkurugenzi wa Halamshauri ya Mlimba, ndg.Jamary Idrisa kwa usimamizi mzuri wa miradi, ikiwemo mradi huo kisha akamwagiza kuweka utaratibu mzuri ili ujenzi ufanyike usiku na mchana, ifikapo tarehe 15 ya mwezi huu shule zinapofunguliwa, shule hiyo ianze kutumika.

“Pia nataka wakati wa kufungua shule tarehe 15 tuzindue kampeni ya upandaji miti hapa na miti ambayo nataka tupande ni michikichi, mikokoa na mikarafuu. Lakini pia nataka migomba ya ndizi ipandwe shuleni hapa ili baadae ije kuwa chakula kwa wanafunzi” alieleza mhe. Kyobya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba ambaye pia ndiye Diwani wa Kata ya Igima, mahali panapojengwa shule hiyo, mhe. Innocent Mwangasa, amemshukuru mhe. Mkuu wa Wilaya kwa ushirikiano mzuri katika usimamizi wa miradi na amesema uwepo wa shule hiyo unakwenda kuondoa utoro na adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shule, ambapo hivi sasa wanalazimika kutembea umbeali wa kilomita takriban saba kwenda shule ya Sekondari Mbingu.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mlimba ameahidi kuweka mazingira wezeshi ili kufanikisha ujenzi kufanyika usiku na mchana nao mafundi wanao tekeleza ujenzi huo, wamesema wako tayari kujenga usiku na mchana ili shule ikamilike kwa wakati tarajiwa.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    February 28, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI WA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA-MLIMBA

    February 08, 2025
  • MLIMBA YAPOKEA MRADI WA MIAKA 5 WA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    February 07, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa