• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

DC KYOBYA AZINDUA MNADA WA KAKAO WA KWANZA KUWAHI TOKEA MLIMBA

Posted on: June 13th, 2024

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero mhe. Dunstan Kyobya amezindua mnada wa kwanza wa mtandaoni, wa Kakao ya wakulima wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba uliofanyika kwenye ghala la Chama cha Msingi cha Wakulima (AMCOS) lililopo kata ya Mbingu, tarehe 12.06.2024 asubuhi.

Katika mnada huo jumla ya kilo 43,750 za Kakao zimeuzwa kwa bei ya shilingi 25,720 kwa kilo, kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani unaoratibiwa na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

Akizungumza na wananchi waliofika ghalani hapo kushuhudia mnada, mhe. Kyobya amehimiza wananchi kuongeza bidii katika kilimo cha mazao ya kimkakati ya mkoa wa Morogoro huku akiyataja kuwa ni Kakao, Karafuu, Chikichi, Kahawa, Pamba na Ufuta.

Vilevile, mhe. Kyobya amepiga marufuku ununuzi wa Kakao mbichi na usafirishaji wa zao hilo nje ya Halmashauri ya Mlimba kama halijapitia kwenye mfumo wa Serikali wa Stakabadhi Ghalani.

Amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtu ye yote atakayebainika kukiuka maagizo hayo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba mhe. Innocent Mwangasa amesema kufanyika kwa mnada huo ni kutimia kwa ndoto ya muda mrefu ya Halmashauri kuwa na minada ya mazao mbalimbali ya biashara yanayo zalishwa ndani ya Halmashauri hiyo.

Amesema Halmashauri imetenga shilingi milioni 70 kwa ajili ya kununua miche ya Kakao ambayo itagawiwa bure kwa wananchi ili waweze kuiotesha kwenye mashamba yao.

Pia amesema wao kama Halmashauri wamejiandaa kuwapa elimu ya kutosha wakulima na amewaagiza maafisa ugani kuhakikisha wanamfikia mkulima mmoja mmoja na kuwapa elimu kwa vitendo ili watakapopata miche hiyo waweze kuiotesha na kuihudumia vizuri hatimaye ilete mavuno mazuri.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba ndugu Jamary Idrisa Abdul amewapongeza wakulima kwa kujitokeza kushiriki mnada huo na kuahidi kuendelea kuhamasisha zaidi kilimo cha zao hilo ili mbeleni minada itakayo kuja ielete fedha nyingi zaidi kwa wananchi na Halmashauri kwa ujumla.

Naye mmoja wa wakulima wa Kakao Wilayani Mlimba, ndugu Calista John Ngasakwa amesema yeye pamoja na wakulima wenzake wamehamasika sana na mnada wa leo kwani kwa mara ya kwanza kabisa tangu waanze kulima Kakao, wameiuza kwa bei yenye tija kubwa (25,720), awali walikuwa wakiuza kilo moja ya Kakao kwa shilingi elfu 3,500 hadi 3,800.


Kupitia mnada wa leo, wakulima wameweza kupata jumla ya shilingi 1,125,250,000 na Halmashauri imepata shilingi 33,757,500, fedha ambayo kwa mujibu wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), inaingizwa moja kwa moja kwenye akaunti za wakulima na akaunti ya Halmashauri pia.

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa