• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

KUMBUKUMBU YA MWL NYERERE KILOMBERO

Posted on: October 14th, 2017

SERIKALI kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya ya Kilombero imeahidi kuwasaidia wanawake kupitia jukwaa la wanawake kwa kuwaunganisha na Taasisi na Asasi mbalimbali ili kuwapatia mafunzo yatakayosaidia kuwakomboa kiuchumi.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu katibu mkuu wizara ya elimu,sayansi na teknolojia Dk Ave Maria Semakafu wakati wa kongamano la jukwaa la wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero ambalo lilikwenda sambamba na maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere yaliyofanyika katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa wilayani hapa.

Dk Semakafu alisema amefurahishwa kuona jukwaa la wanawake linafanya kazi yake ipasavyo katika wilaya hiyo kwa kuwaunganisha wanawake katika kata zote na kusema kuwa dhana nzima ya majukumu ya wanawake ni kurejea misingi ya ujamaa.

Alisema katika kuwaunga mkono wanawake wa halmashauri hiyo atahakikisha wanapata mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali na kwa kuanzia watawachukua wanawake wachache kwa ajili ya mafunzo na hao wachache wakirudi watakwenda kuwafundisha wenzao.

Hata hivyo naibu katibu mkuu huyo aliwaagiza wanawake hao kuhakikisha wanakaa na kujihudumia kiujamaa na pia wajitengenezee mitaji ili waweze kukopesheka sambamba na kuwachunga watoto wao wa kike wasipate mimba wakiwa mashuleni.

Awali mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya ya Kilombero Bi Amina Mrisho alitaja changamoto wanazokabiliana nazo wanawake wa wilaya ya Kilombero kuwa ni pamoja na kukosa elimu ya ujasiliamali, utambuzi wa fursa zilizopo maeneo yao, kukosa mitaji, uelewa wa sheria na haki zao na pia unyanyasaji wa kijinsia na mimba za utotoni.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Dennis Londo alisema kuwa wao wameona umuhimu kuadhimisha siku hiyo katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa  kutokana na Hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kushiriki kukiasisi Kijiji hicho kama Kijiji cha ujamaa cha mfano ambacho nacho bado kinasimamia falsafa ya baba wa taifa katika dhana ya ujamaa kwa kumiliki kwa pamoja mashamba makubwa na magari.


Matangazo

  • KARIBUNI MLIMBA WATUMISHI WAPYA SEKTA YA ELIMU NA AFYA July 04, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 25, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • AFISA LISHE WA HALMASHAURI NDUGU BODYGADI S. BUHARI AKIWASILISHA TATHIMINI YA LISHE KWA MWAKA 2021/2022

    July 15, 2022
  • UJENZI WA NYUMBA ZA WAKUU WA IDARA

    July 04, 2022
  • KARIBUNI MLIMBA WAAJIRIWA WAPYA SEKTA YA AFYA NA ELIMU

    July 04, 2022
  • Ujenzi wa Kituo cha Afya Igima wafikia hatua nzuri.

    June 07, 2022
  • Angalia zote

Video

MAKAO MAKUU KILOMBERODC KUHAMIA MNGETA
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa