• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MIFUGO YOTE ISIYOWEKWA ALAMA MWISHO WA KUTAMBULIWA KILOMBERO NI MACHI 31 MWAKA HUU- DC

Posted on: March 25th, 2017

MKUU Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo amesema kuwa baada ya Machi 31 mwaka huu Mifugo iliyosajiliwa NA kuwekwa alama ndiyo itajayotambuliwa wilayani humo na isiyokuwa NA alama itabidi iondolewe lasivyo itataifishwa.

Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuzungumza na viongozi na wafugaji wa vijiji vya Bwawani,Nyamwezi na Kiberege katika kata ya Kiberege wilayani hapa.

Ihunyo alisema kwa sasa katika maeneo mbalimbali wilayani humo kuna makundi makubwa ya mifugo yanaingia kinyemela huku baadhi ya wafugaji wakificha Mifugo yao NA kukataa kuwekwa alama NA kusema kuwa serikali yake haitokubali Wilaya hiyo kuwa dampo la Mifugo kwa sasa.

Alisema hairuhusiwi kwa Mifugo kuingia katika Wilaya hiyo kwa sasa labda kwa mamlaka ya Afisa Mifugo Wilaya ambaye ndie mwenye mamlaka ya kutoa kibali NA kutoa rai kwa viongozi wote kuanzia ngazi za vitongoji hadi kata kutoa taarifa punde wanapoona makundi ya Mifugo yakiingia maeneo yao.

Aidha Mkuu huyo Wa Wilaya amewaagiza diwani na Mtendaji kata Wa Kiberege kwa kushirikiana na maafisa Ardhi kukagua kisha kutoa ekari 1000 za Ardhi ambazo zilitolewa enzi ya kijiji kimoja cha Kiberege kwa wafugaji ambapo toka mwaka huo hadi Leo hazijatolewa.

Kuhusu kutatua migogoro ya wakulima NA wafugaji,Ihunyo aliziagiza serikali za vijiji kubainisha maeneo yao NA kutenga maeneo ya wafugaji kama yatakuwepo NA pia wakitengeneza njia kwa ajili ya kunyweshea Mifugo sambamba NA kutengeneza malambo.

Amebainisha kuwa viongozi wengi Wa vijiji wamekuwa ndio vyanzo vya migogoro katika maeneo yao hivyo kuwataka wabadilike lasivyo atakaebainika atamshughulikia.

Awali jamii ya wafugaji wanaoishi katika kata hiyo walilalamikia viongozi Wa vijiji kutowapatia eneo la ekari 4623 walizopewa NA kijiji kimoja enzi hizo kinaitwa Kiberege kabla ya sasa kuwa NA vijiji vitatu vya Kiberege,Nyamwezi na Bwawani.

Mmoja Wa wafugaji hao Kazingoma Kushonga alisema eneo la wafugaji lilitengwa toka mwaka 2003 NA kukamilika mwaka 2004 katika kukamilisha Mpango Wa matumizi bora ya Ardhi ambapo walichangia shilingi milioni moja ili kukamilisha Mpango huo.

Kushonga alisema baada ys zoezi kukamilika walikuwa wakisubiri kukabidhiwa eneo lao lakini wamezungushwa toka kipindi hicho hadi Leo licha ya uongozi Wa mkoa kuagiza wafugaji hao kupewa eneo lao.

Naye Bony Nangeleki alisema wakati wakiendelea kusubiri eneo lao wakashangaa katika mkutano Wa January 13 mwaka huu vijiji vyote vitatu kudai kuwa hawana eneo la wafugaji wakati wao wanaelewa eneo lao lipo katika vijiji vipya vya Nyamwezi na Bwawani ambapo hivi sasa maeneo hayo yamelimwa NA wakulima.

Ndipo diwani Wa kata ya Kiberege Shabani Mlango alipoinuka NA kusema kuwa kweli enzi ya kijiji kimoja wafugaji waliomba eneo la ukubwa huo lakini wananchi waligoma kutoa ekari hizo 4623 na kubariki ekari 1000 tu tokana NA uchache Wa wafugaji kuwa sita tu.

Mlango alisema lakini baadae ekari hizo 1000 zikaleta mgogoro baada ya mfugaji mmoja kudai ekari zake 460 alizonunua kijijini na alishinda kesi hivyo wao kuamua kugawa ekari 460 katika ekari 1000 walizotenga NA baada ya vijiji kugawanyika zikaonekana ekari hizo 1000 zipo katika kijiji cha Bwawani.

Baada ya Maelezo hayo Mkuu Wa Wilaya aliagiza uongozi Wa kata NA wataalamu Wa Ardhi kubainisha hizo ekari 1000 NA kisha kugawa ekari 460 kwa mfugaji  pale watakapojirisha hukumu iliyotolewa NA ekari nyingine 540 wapewe wafugaji ili kumaliza mgogoro huo.

Hatahivyo wafugaji hao bado walipingana NA maagizo ya Mkuu Wa Wilaya kwa kusema kuwa kwa kufuata haki basi wanatakiwa kupewa ekari 1000 kama walivyokubaliwa NA mkutano Wa kijiji NA ekari 460 za mfugaji aliyeshinda kesi kijiji kinatakiwa kimpatie nje ya eneo hilo kwani alizinunua kihalali NA sio maombi ya wafugaji.

Mwisho....

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa