• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Maadhimisho ya mtoto wa Afrika yafana Mlimba.

Posted on: June 17th, 2021

Pichani juu: mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mlimba Mh. Innocent Mwangasa akiongea na baadhi ya washiriki (Hawapo pichani) kuhusiana na siku ya mtoto wa Afrika

Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika hapo jana yamefana kwa kiasi kikubwasana katika Halmashauri ya wilaya ya Mlimba ambapo Watoto mbalimbaliwalishiriki katika kuonesha vipaji mbalimbali na kufundishwa mambo mbalimbaliyanayohusiana na haki zao, katika upande mwingine wazazi wamekumbushwa namnabora ya kuwalinda Watoto wao ili wasipate matatizo yoyote katika Maisha yao nakufanikisha ndoto zao bila kikwazo chochote kile.

Hayo yamesemwa na kaimu Mkurugenzi Dr. Christina Guvetti alipokuwa akitoasalamu za mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.

Dr. Guveti ameongeza kuwa Halmashauri, CAMFED Pamoja na Plan Internationawaliandaa mikakati mbalimbali juu ya ulinzi wa mtoto aliyepo katika Halmashauriya wilaya ya Mlimba, mipango Madhubuti pia imefanywa kwenye suala la elimu nahilo limefanikiwa kuleta mabadiliko makubwa sana mfano kwa mwaka 2019 kiwangocha ufaulu kilikuwa ni 86.6% wakati 2020 kiwango kiliongezeka na kufikia 95.3%.

Katika hatua nyingine Dr. Guveti alisema kuwa wazazi wasikubali Watoto waokuishia kidato cha nne pekee, kwani kwa sasa Halmashauri imefanya jitihada zakusajili shule mbili ya Nakaguru na Kiburubutu kufundisha Watoto wa kidato chatano na sita, hivyo hii ni fursa kwa Watoto wa Halmashauri hii, shule hiiisiachwe kwa wanafunzi wanaotoka nje ya Halmashauri kuja kujaza shule hizi,wanafunzi wa hapa wanatakiwa kujitahidi kwa kila hali kufanya vizuri ili wawezekupata nafasi hapahapa nyumbani.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mlimba ambae pia ni Diwani wakata hiyo ya Igima Mh. Innocent Mwangasa amesema kuwa anaungana na Mkurugenzikwa kuwaasa wazazi waanze wao kuwalinda watoto wao kisha wengine wafuate, nawale ambao wamezoea kuwanyanyasa Watoto wakae chonjo kwani dawa yao inachemka.

Akiendelea kusisitiza, Mh. Mwangasa amesema kuwa walimu wakuu wote katikaHalmashauri hiyo ambao wana tabia ya kushirikiana na wazazi na wahalifu kufichauovu wa kuwapa ujauzito Watoto, walimu hao hawana nafasi kwenye shule zilizokokwenye Halmashauri yake na ataanza kuwachukulia hatua kali za kinidhamu ikiwamokufukuzwa kazi kwani wao ndio chanzo cha Watoto kufanyiwa ukatili wa kinyamakatika jamii zao.

Siku ya mtoto wa Afrika, huadhimishwa kila mwaka barani Afrika kupingamauaji na ukatili waliofanyiwa Watoto wa huko Afrika kusini na makaburu, mauajihayo yalifanyika katika kitongoji cha SOWETO mwaka 1976 wakati Watoto haowalipokuwa wakiandamana kudai Haki zao za msingi.

Habari Picha.

Pichani chini mwenyekiti wa baraza la watoto la wilaya ya Mlimba akiongea jambo na watoto wenzake pamoja na wageni waliohudhuria kwenye maadhimisho hayo

pichani mgeni Rasmi ambae ni kaimu Mkurugenzi Dr. Christine Guveti akiwa Mwenyekiti na Katibu wa baraza la vijana katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika mapema janaWageni mbalimbali waliohudhuria katika shughuli hii ya siku ya Mtoto wa Afrika

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa