• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MKURUGENZI JAMARY AKAGUA MIRADI INAYOENDELEA KUTEKELEZWA NA HALMASHAURI YAKE

Posted on: December 24th, 2024

Na, Milka Kaswamila-Mlimba DC

Halmashauri ya Wilaya Mlimba inajivunia maendeleo makubwa ambayo inaendelea kuyatekeleza katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya afya, elimu ya awali, msingi, sekondari, na kwa kuendelea kuhakikisha utekelezaji wa miradi unafanyika kwa viwango vya juu.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mlimba, ndg. Jamary Idrisa Abdul amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi inayoendelea kutekelezwa ndani ya Halmashauri hiyo.

Katika ziara hiyo, amekagua miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Zahanati ya Chiwachiwa, ujenzi wa wodi tatu katika Hospitali ya Halmashauri, ukamilishaji wa wodi tatu za upasuaji, ujenzi wa nyumba tatu kwa moja za watumishi wa afya na ujenzi wa shule mpya ya sekondari katika Kata ya Igima, huku akitoa maelekezo ya kuboresha na kuhakikisha utekelezaji wa miradi unaendelea kama ilivyo pangwa.

Aidha, Mkurugenzi Jamary ameeleza kuridhishwa na jitiihada zinazofanywa na mafundi pamoja na wasimamizi wa miradi hiyo, za kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa ubora na kwa haraka, huku akisisitiza umuhimu wa usimamizi mzuri na uwazi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

“Kwa sasa Halmashauri ya Mlimba tunatekeleza miradi nane katika sekta ya elimu ya sekondari, miradi 27 sekta ya elimu ya awali na msingi, na miradi 13 katika sekta ya afya.

Vilevile, Halmashauri ilitenga shilingi 100,000,000.00 kutoka katika mapato yake ya ndani ili kutengeneza viti na meza 1,818 kazi ambayo inatazamiwa kukamilika hivi karibuni ili Januari 2025 shule zitakapo funguliwa, samani hizo ziweze kutumika shuleni.


Miradi hii ni muhimu kwa maendeleo ya wananchi wa Halmashauri ya Mlimba na tutahakikisha kwamba kila mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwa maslahi ya jamii. Sisi Halmashauri pamoja na Serikali Kuu, tunalenga kuboresha maisha ya wananchi wetu kwa kutoa huduma bora na miundombinu imara" alieleza kwa kina Mkurugenzi Jamary.

Halmashauri ya Wilaya Mlimba inaendelea kufanya juhudi za kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na inakuwa na manufaa kwa jamii, ikiwa ni sehemu ya harakati za serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuboresha maisha ya wananchi.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa