Pichani juu: Mkuu wa Mkoa wa Morogoro mheshimiwa Kebwe Steven Kebwe akizungumza katika baraza maalum la majibu ya hoja za ukaguzi wa mthibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali mwaka wa fedha unaoishia 30,juni,2018.
MKUU wa Mkoa wa Morogoro mheshimiwa Kebwe Steven Kebwe,ametoa agizo mapema leo kwa wale wote wasioweka benki pesa ambazo walikusanya kutoka katika vyanzo vya mapato mbalimbal, wakamatwe ili iwe fundisho kwa wengine na kumtaka mwenyekiti na madiwani wasimamie vyema na kikamilifu suala zima la mapato.
Mheshimiwa Kebwe ametoa agizo hilo pindi alipokuwa katika mkutano wa baraza maalum la majibu ya hoja za ukaguzi wa mthibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali mwaka wa fedha unaoishia juni 30 2018,uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Aidha Kebwe amesema kuwa sio jambo zuri sana kwa Halmashauri iliyo Tajiri kama Halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuendelea kuwachangisha watu maskini miradi mbalimbali.
“Hatuwezi kuwa na Halmashauri Tajiri halafu tuendelee kuchangisha watu maskini kwa miradi,”alisema mheshimiwa Kebwe kwa lengo la kuzitumia ipasavyo rasilimali zilizopo ndani ya Halmashauri ya Kilombero ili kuweza kusaidia upatikanaji wa mapato kwa urahisi.
Hatahivyo Mkuu wa Mkoa amaetoa rai kwa Hlmashauri ya wilaya ya Kilombero kuanzisha miradimipya kama vile kuwa na kiwanda cha sukari kitakachomilikiwa na Halmashauri yenyewe pamoja na kilimo, na hiyo ni kutokana na kuwepo kwa eneo kubwa ndani ya Halmashauri hiyo na sio kujikita katika soko na stendi pekeyake ili kuweza kusaidia kuboresha mfuko wa vyanzo vya mapatokwa ujumla.
Mngeta Kijiji cha Itongoa
Anuani: P.O.BOX 263
Simu: 023 293 1523
Mobile: 0232931523
Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa