• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

PANYA WAHARIBIFU WA MAZAO WADHIBITIWA KILOMBERO

Posted on: January 16th, 2018

BAA la uharibifu wa mazao limejitokeza katika wilaya ya Kilombero baada ya panya waharibifu wa mazao kushambulia mazao ya mpunga na mahindi na kusababishia hasara wakulima.

Panya hao wameanza uharibifu huo tokea Novemba mwaka jana ambapo walianza kuonekana katika kata za Mwaya na Mngeta katika halmashauri ya wilaya ya Kilombero na kisha kuonekana katika kata nyingine katika halmashauri zote mbili za Kilombero na mji wa Ifakara.

Hata hivyo juhudi za halmashauri hizo mbili katika kuwadhibiti panya hao zilifanikiwa ambapo halmashauri hizo ziliamua kununua sumu na kuweza kuwateketeza panya hao japo kuna baadhi ya maeneo bado wanaendelea kusumbuliwa na wadudu hao waharibifu.

Mkurugenzi wa mji wa Ifakara Francis Ndulane alisema baada ya kupata taarifa mapema mwezi huu aliamua kuwasiliana na mkurugenzi mwenzie wa wilaya na kuelezwa kuwa tatizo hilo lilianzia katika halmashauri hiyo kwa mashamba ya mahindi kuharibiwa katika kata ya Chita.

Ndulane alisema lakini siku chache alipewa taarifa kuwa maeneo jirani na halmashauri yake huko Idete wamevamia panya hao na baadae kusambaa katika vijiji viwili vya halmashauri yake ambavyo ninIhanga na Lumemo.

Alisema baada ya kubaini uvamizi huo katika halmashauri yake walipanga mkakati na halmashauri ya wilaya ya Kilombero ili kuweza kuwadhibiti panya hao na kupeleka taarifa mkoani na baadae kuamua kununua sumu ili kuweza kuwaangamiza panya hao.

Mkurugenzi huyo wa mji alisema katika ununuzi wa sumu hiyo halmashauri ya wilaya Kilombero walinunua kilo 50 na halmashauri ya mji walinunua kilo 10 na kazi ya usambazaji wa sumu hiyo ulianza na maeneo mengi katika halmashauri ya mji wamefanikiwa kuwaangamiza panya hao.

Ndulane alisema kwa sasa wataalamu wa kilimo katika halmashauri hiyo wamesambaza sumu maeneo yote yaliyoathirika na pia wanahamasisha wakulima kutumia njia za kienyeji ili kuwadhibiti panya hao ambapo kwa namna moja ama nyingine wamefanikiwa.

Naye Afisa Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero Mohamed Ramadhani alisema kwa sasa hali ni shwari katika maeneo mengi wilayani humo kwani waianza kugawa sumu toka Januari 6 mwaka huu na tatizo hilo lilianza kubainika wilayani humo toka Novemba mwaka jana.

Ramadhani alisema ekari zaidi ya 300 zimeharibiwa na panya hao na kubainisha kuwa licha ya kusambazwa kwa sumu katika maeneo yaliyoathirika pia mvua zilizoanya kunyesha hasa maeneo ya mabondeni zimesaidia kuua panya hao ambapo kwa hivi sasa wataalamu wanaendelea kutembelea maeneo mbalimbali ili kuwamaliza kabisa panya hao.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa