• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

RC BATILDA AWAALIKA WAFUGAJI NANENANE KANDA YA MASHARIKI

Posted on: August 2nd, 2024

Na, Milka Kaswamila-Mlimba DC

Maonesho ya Wakulima (Nanenane) Kanda ya Mashariki yamezinduliwa leo tarehe 02.08.2024 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga mhe. Batilda Burian, kwenye Uwanja wa Mwalimu Nyerere Nanenane Morogoro.

Akizungumza na hadhira iliyo kuwepo wakati wa uzinduzi huo, mhe. Batilda amewaalika wafugaji waje kwenye maonesho wajifunze aina za malisho ambayo yanaweza kulimwa kwenye eneo dogo lakini yakalisha mifugo mingi.

Mhe. Batilda amesema elimu hiyo itasaidia wafugaji kuweza kufuga kisasa na kuepuka ufugaji holela wa kuhamahama ambao unachangia sana kuwepo kwa migogoro kati ya wakulima na wafugaji pindi mifugo inapoingia kwenye mashamba ya wakulima na kula mazao.

Vilevile, mhe. Batilda amepongeza Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) pamoja na wanafunzi wake walio gundua na kutengeneza application ya kutambua afya ya mnyama mmoja mmoja wawapo bandani.

“Hongera sana SUA na vijana wetu kwa kugundua hilo na tunaomba mpite kwenye maeneo yetu kuzungumza na wafugaji wetu kuhusu teknolojia hiyo” alieleza mhe. Batilda.

Kwa upande wa kilimo, mhe. Batilda amemshukuru Rais Samia kwa kuwezesha maafisa ugani wa Halmashauri zote nchini kupata pikipiki na vyombo vya kupima afya ya udongo ili kuimarisha  shughuli za kilimo kwenye maeneo yao ya kazi.

Pia, mhe. Batilda amewataka wakulima wajifunze na kubadilisha aina za kilimo kwa kufanya kilimo cha umwagiliaji, vitalu nyumba na ufuatiliaji wa teknolojia za kisasa ili waweze kujikomboa zaidi kiuchumi.

Mhe. Batilda amesema mikoa ya Kanda ya Mashariki (Pwani, Morogoro, Dar-es-Salaam na Tanga) ina kila sababu ya kufanya vizuri zaidi katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya masuala ya kilimo mifugo na uvuvi kwa sababu Taasisi za Tafiti za sekta hizo zimo ndani ya kanda hiyo kama vile SUA Morogoro, TARIRI Tanga na Taasisi ya tafiti za uvuvi huko Kunduchi Dar-Es-Salaam.

Akizungumzia Kauli Mbiu ya Maoenesho ya Nanenane ya mwaka huu, mhe. Batilda ametoa wito kwa  wakulima, kushiriki kikamilifu kujitokeza kugombea  na kuchagua viongozi bora watakao himiza shughuli za kilimo.

“Kiongozi ni lazima aoneshe mfano ili wananchi wake waweze kujifunza kutoka kwake” alisema mhe. Batilda.

Aidha, mhe. Batilda amesema sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi zimetoa ajira kwa zaidi ya asilimia 65, zimechangia pato la Taifa kwa zaidi ya asilimia 28 na zinachangia usalama wa chakula na lishe bora kwa wananchi.

Ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuimarisha miundombinu ya sekta hizi ikiwemo kuanzisha skimu za umwagiliaji, kuanza kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za ufugaji, kuimarisha Benki ya Kilimo na miundombinu ya usafiri na usafirishaji.

Kauli Mbiu ya Maonesho ya Nanenane mwaka huu inasema “Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”.

MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa