• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

SIGNAL, SULULU NA SAGAMAGANGA WANUFAIKA NA MRADI WA UPIMAJI NA URASIMISHAJI(LTSP) BAADA YA KUMALIZA MIGOGORO KATI YAO

Posted on: January 12th, 2018

VIJJI vitatu vya Signali, Sululu na Sakamaganga vilivyopo kata ya Signal wilaya ya kilombero mkoani Morogoro vimemaliza mgogoro mkubwa wa mipaka yake na hivyo kuwa kwenye fursa ya kunufaika na mradi wa upimaji na urasimishaji ardhi (LTSP).

Wilaya za Kilombero,Malinyi na Ulanga ni wilaya tatu zilizochaguliwa kutekeleza zoezi la upimaji na urasimishaji wa ardhi kwa majaribio katika mkoa wa Morogoro lengo kuu likiwa ni kupanga matumizi bora ya ardhi ili kupunguza migogoro na ugomvi  baina ya wakulima na wafugajii.

Akitoa taarifa hiyo kwa katibu mkuu wa ardhi,Nyumba na maendelea ya makazi Doroth Mwanyika  aliye ziarani wilayani humo kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo,kupitia mkutano na wanakijiji cha kwenye mkutano wa wanakijiji cha Sakamaganga,Mkuu wa wilaya ya Kilombero James Ihunyo alisema mgogoro huo umemalizika baada ya vikao Zaidi ya vitano vilivyofanyika na wanavijiji hao kwa nyakati tofauti.

Alisema kuwa kutokana na mgogoro huo,timu ya wapimaji kutoka mradi wa upimaji na kurasimisha ardhi ilishindwa na kuendelea na zoezi lake la upimaji ardhi ya vijiji hivyo.

“Nafurahi kuutangazia umma mbele yako katibu mkuu, kuwa ule mgogoro wa mipaka wa vijiji vitatu umeisha na kwahiyo lile zoezi lililosimama kwa muda la upimaji wa ardhi na baadaye kuurasimisha ardhi linaweza kuendelea,”alisema Ihunyo.

Ihunyo aliendelea kusema kuwa ofisi yake iko kwenye hatua ya kumalizi mogogoro mwingine wa ekari 60 baina ya wawekezaji binafsi na Kijiji cha sekamagamba ambapo timu ya wataalam wa sheria wakishirkiana na maafisa ardhi wa manispaa wanashughulikia.

“Nimeshaagiza timu ya waataalam wa sheria kutoka ofisi yangu washirikiane wa maafisa ardhi kulishughulikia tatizo hilo ili haki iweze kutendeka kwa pande zote mbili za mgogoro,”alifafanua mkuu huyo wa wilaya.

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya amewahakikishia wananchi wa vijiji jirani na barabara itokayo kidatu mpaka Ifakara kuwa hakuna mkazi nyumba yake itabomolewa kupisha upanuzi wa barabara bila kulipwa.

Alisema zoezi liko wazi na tathmini inaendelea kuafanya na timu ya wataalam kutoka  wakala wa barabara(TANROAD)  wakishirikia na wa maeneo husika inapopita barabara hiyo ambayo itajengwa kwa kiwango cha lami.

Akihutubia wananchi hao,Katibu mkuu wa wizara ya ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi Dorothy Mwanyika aliwataka wanavijiji hao kutumia fursa mbalimbali zinazotopatikana kupitia mradi wa upimaji na urasimisha ardhi ili kujiletea maendeleao ngazi ya familia,Kijiji na taifa kwa ujumla.

Alisema migogogo ya ardhi ni chanzo kikubwa cha kudorora kwa maendeleo maeneo husika kutokana na muda mwingi kutumika kukashughulika kutatua migogoro hiyo na kutumia muda mchache kwenye  shughuli za maendeleao.

“Nawashukuru kwa kuwa tayari kumaliza migogogro na hivyo nawaomba kutumia fursa za mradi huu ili kuweza kujiletea maendeleao yenu wenye kwenye kaya,Kijiji na hata taifa kwa ujumla.Ardhi yako ikipimwa, thamani yake inaongezeka maradufu,” Mwanyika alisema.

“Natoa mwito kwa timu ya wapima kuanza zoezi hili mara moja ili kukamilisha zoezi katika vijiji hivyo vitatu na hatimaye waweze kukabidhiwa hati zao za kimila baadae.Mtoe ushirikiano kwa wapimaji ili zoezi liweze kwenda kwa haraka Zaidi.

Kwa upande wake mkazi wa Kijiji hicho Isa Lupia alimwomba katibu mkuu kuhakikisha kuwa zoezi la upimaji lingalie pia namna gani wanavijiji watanufaika na miradi iliyopo ndani ya eneo la Kijiji chao ikiwemo mgodi wa machimbo yam awe.

Alisema imefikia wakati na wao  kama wanakijiji kunufIKA  miradi mikubwa kama hiyo imayoendelea Kijiji hapo  kama ujenzi wa shule na zahanati kama maeneo mengine wanavyonufaika na miradi kama hiyo.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI February 24, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MATUMIZI YA KAWAIDA JULAI 2022 August 01, 2022
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA IMEPOKEA PESA ZA MATUMIZI YA KAWAIDA KUTOKA HAZINA (OC) KWA MWEZI NOVEMBA 2022 TSHS 35,294,000/= December 05, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA KAMATI YA SHEREHE WILAYA

    May 23, 2023
  • FEDHA ZA OC KWA MWEZI FEBRUARI 2023 TSH. 35,294,000

    March 16, 2023
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA OC KWA MWEZI JANUARY TSH. 189,174.000/=

    February 07, 2023
  • MHE. DUNSTAN KYOBYA MKUU WA WILAYA YA KILOMBERO ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI NAKAGURU

    February 02, 2023
  • Angalia zote

Video

MHE. WAKILI DUNSTANI KYOBYA AHAIDI TSH. 500,000.00/= KWA KILA MWANAFUNZI ATAKAYEPATA DIVISHENI 1.7.
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa