• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

TAARIFA YA MAENDELEO YA KILIMO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO 2018

Posted on: March 1st, 2018


Kwa mujibu wa Afisa Kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero ndugu Mohammed Ramadhani juu pichani, ifuatayo ni taarifa fupi ya hali ya kilimo katika halmashauri ya wilaya ya kilombero 

kama alivyoongea na Afisa habari wa Halmashauru hiyo ndugu ISLAM MPOSSO

1.0 Hali ya chakula Wilaya ya Kilombero Feb 2018

Kwa mujibu wa Sensa ya watu  na makazi 2012 Wilaya ya Kilombero ina wakazi wapatao 407,880 na jumla ya kaya 94,604. Ongezeko la idadi ya watu kwa mwaka ni asilimia 2.4, hivyo kadirio la idadi ya watu kwa mwaka 2016/17 ni Halmashauri ya Wilaya kuwa na watu 344,410. Mahitaji halisi ya chakula mchanganyiko kwa mwaka itakuwa ni tani 138,194 (tani 124,374.6 za chakula aina ya wanga na tani 13,819.4 za chakula aina ya utomwili).   Utekelezaji wa malengo/uzalishaji 2016/17 ni tani 572,664 hivyo  ikiwa ni ziada ya tani 434,470.Hivyo Halmashauri ina chakula cha kutosha na hakuna tishio la njaa katika ujumla wake.

1.1. Upatikanaji wa Chakula na Bei zake 

Upatikanaji wa chakula ni mzuri kwa ujumla, isipokuwa bei ya baadhi ya vyakula hasa mchele imepanda katika kipindi hiki kwa sababu baadhi ya maeneo mengi ya nchi hayakuzalisha chakula cha kutosha. Hali hii imesababisha wanunuzi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi kuja kununua mchele kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero lakini hali iko tofauti katika zao la mahindi bei imeendelea kupungua hadi kufikia Tsh.10,000 kwa debe kwa bei ya juu na chini ni 5,500. Tazama jedwali No.1 hapo chini:-

Jedwali Na.1: Bei ya Mazao Sokoni.


Na
Aina ya Chakula
Upatikanaji wa
Chakula Sokoni
Kinakopatikana
Bei ya
chini kwa 
kilo/Tsh.
Bei ya 
juu kwa 
kilo/Tsh.
Kinapatikana/
Hakipatikani
Ndani ya
wilaya
Nje ya 
Wilaya
1
Mahindi
Kinapatikana
√

306
556
2
Mpunga
Kinapatikana
√
 
533
867
3
Ngano
Kinapatikana

√
2,000
2,500
4
Mtama
Kinapatikana
√
√
1,800
2,000
5
Ulezi
Kinapatikana

√
1,500
2,500
6
Uwele
Kinapatikana

√
2,000
2,500
7
Makopa
Kinapatikana
√
√
1,600
2,200
8
Mhogo mbichi
Kinapatikana
√

650
1,150
9
Viazi vitamu
Kinapatikana
√
√
950
1,150
10
Viazi Mviringo
Kinapatikana

√
1,000
1,250
11
Ndizi
Kinapatikana
√

850
1,050
12
Maharage
Kinapatikana

√
1,800
2,400
13
Mikunde mingine
Kinapatikana
√
√
1,500
1,800


Nb. Mchele bei ya chini ni Tsh.1,450 na ya juu ni 2,000 kwa kilo.

      Unga wa Mahindi bei ya chini ni Tsh. 1,000 na ya juu ni 1,250 kwa kilo.

Halmashauri ya Wilaya inaendelea kuhamasisha Wananchi kuwa na tabia ya kuhifadhi chakula cha kutosha kwa ajili ya matumizi ya mwaka mzima kwa:-

Kutoa elimu ya matumizi sahihi ya chakula.

Kupanua wigo wa kulima mazao mengine badala ya chakula badala ya kutegemea zaidi zao la mpunga.

Kuhimiza wananchi kupanda mazao yanayokomaa kwa muda mfupi na yanayostahimili ukame.

-Kuhimiza wakulima walioko katika maeneo ya umwagiliaji kuendelea kuzalisha zaidi ya mara moja kwa mbinu ya mazao mchanganyiko pale inapoonekana maji hayatoshelezi kulima mpunga eneo lote.

1.2. Hali ya Hewa

 Kwa msimu 2017/18 mvua zimeanza kunyesha kwa muda muafaka, japo hazina matawanyiko mzuri lakini tayari kazi muhimu za maandalizi ya mashamba, upandaji na utunzaji wa mimea iliyopo shambani unaendelea. Katika mwezi Februari kumekuwa na upungufu mkubwa wa mvua kulikopelekea baadhi ya maeneo yaliyopandwa zao la Mahindi kuathirika kwa kukosa unyevu wa kutosha kuzalisha. Tazama jedwali Na.2. linaloonesha mwanguko wa Mvua kwa kituo kilichopo bomani;-

 

Jedwali Na.2 Mwanguko wa Mvua - Msimu 2017/2018 hadi Feb 25 2018

Mwezi
Sept
Octoba
Nov
Disemba
Januari
Februari
Jumla mm.

0

0

49.8

137.9

261.4

2.7

Idadi ya Siku

0

0

6

5

9

1

2.0.    Hali ya Uzalishaji wa Mazao ya Chakula

Utekezezaji wa malengo ya Kilimo kwa mwaka umekuwa ukiathiriwa sana na mabadiliko ya hali ya hewa hasa mvua ambazo zimekuwa si zauhakika wa kutosheleza mahitaji ya unyevu kwa mazao yaliyopo shambani. Mvua hizi ama  huchelewa kuanza kunyesha na kusababisha kuchelewa kupanda mazao mashambani na kusababisha mazao kutokomaa vizuri, au zinanyesha nyingi na kuathiri maandalizi ya mashamba, upandaji na mazao yaliyopo shambani.

Yafuatayo ni majedwali yanayoonesha hali halisi ya uzalishaji wa mazao ya chakula katika msimu 2016/2017 pamoja na Utekelezaji na matarajio ya mavuno msimu wa mwaka 2017/18  hadi Jan. 2018:- 

 

Jedwali No.3. Utekelezaji wa Malengo Msimu 2016/17

UTEKELEZAJI WA MALENGO YA KILIMO MSIMU 2016/17

Zao
Malengo kwa mwaka
Utekelezaji 
Mazao ya Chakula
Eneo litakalopandwa (ha)
Matarajio ya mavuno (tani)
Eneo liliopandwa (ha)
Mavuno Halisi (tani)
Mahindi

38,202

95,505

27,885

69,713

Mpunga

108,865

381,027

101,056

353,696

Mtama

629

629

248.6

284.9

Uwele

0

0

0

0

Ulezi

7

4.2

6

6

Mihogo

9,572

191,440

1780

35600

Viazi vitamu

5,873

70,470

2041.6

24417.2

Ndizi mbivu

2,630

78,912

840.2

24346

Ndizi mbichi

4,678

131,880

2168

64130

Kunde

1,657

1,326

415

319.9

Maharage

217

195

152

150.8

Jumla Ndogo

172,330

951,388

136,592

572,664

 




Mazao ya Biashara




Miwa

5,909

472,744

5444.7

277420

Alizeti

912

1,368

24.8

37.3

Ufuta

10,145

10,145

3093.9

3145.5

Kakao

3,112

3,112

1462

1462

Nazi

1,919

13,435

1215.3

8555.1

Jumla Ndogo

21,997

500,804

11,241

290,620






Mazao Mengine




Embe

1,457

21,851

984

12,735

Chungwa

617

9,260

275.9

3,602

Tikiti maji

1,339

26,780

280.4

6,617

Vitunguu

391

7,814

10.4

183

Bamia

796

7,964

125.9

1,240

Nyanya

1,875

16,405

186.5

1,637

Nyanya chungu

1,199

8,994

237

1,807

Chinees Cabbage

847

10,585

142.7

1,812

Jumla Ndogo

8,521

109,653

2,242

29,632

Jumla Kuu

202,848

1,561,845

150,076

892,915

 

 

Jedwali No.5.  Malengo ya Msimu 2017/18

MALENGO YA KILIMO NA UTEKELEZAJI MSIMU 2017/18

Zao
Malengo kwa mwaka
Utekelezaji hadi Jan.2018
Mazao ya Chakula
Eneo litakalopandwa (ha)
Matarajio ya mavuno (tani)
Eneo liliopandwa (ha)
Mavuno Halisi (tani)
Mahindi

28,775

76,793

14,807.2


Mpunga

104,078

371,689

63,945.8


Mtama

1275.4

2353.3

33


Uwele

2

3

0


Ulezi

15

20.5

9.5


Mihogo

6,298

125,954

585.1


Viazi vitamu

4,719

56,599

760.4


Ndizi mbivu

2,436

71,464

1,837.2


Ndizi mbichi

5,306

156,883

4,196


Kunde

2,251

1,700

288.8


Maharage

228

280.8

122


Jumla Ndogo

155,383

863,740

86,585

0

 




Mazao ya Biashara




Miwa

4,029

201,450

3,461.1

Alizeti

1071.6

1,576

8.5

Ufuta

5,726

5,726

796

Kakao

4,691

4,668

595.7

Nazi

904

6,338

563.6

Jumla Ndogo

16,421

219,758

5,424.9

0






Mazao Mengine




Embe

1,083

16,181

960.5

Chungwa

312.6

4,699

211.2

Tikiti maji

488

9,246

161.1

Vitunguu

86.1

1,722

16.5

Bamia

290.9

2,909

160.4

Nyanya

456

4,009

144.8

Nyanya chungu

491

3,681

233.5

Chinese Cabbage

446.9

5,586

139.7

Jumla Ndogo

3,654

48,033

2,011.2

0

Jumla Kuu

175,458

1,131,530

94,021.1

0

 

3.0.    Changamoto za Uzalishaji wa Mazao.

  • Visumbufu vya mazao hasa panya waharibifu wa mazao(imesababisha baadhi ya wakulima kushindwa kupanda mazao wakisubiri tatizo hilo kupungua) na viwavi vamizi (Fall Army Worms).
  • Kutokamilika kwa miundombinu ya umwagiliaji.
  • Tabia ya wakulima wengi kupendelea kulima zao moja yaani mpunga na kutoyapa kipaumbele mazao mbadala kama Mihogo, Viazi na Ndizi.
  • Kuainishwa kwa mipaka ya Hifadhi ya Bonde la Kilombero kumepunguza maeneo ya kilimo cha mpunga.
  • Mvua tata (Unyeshaji wa mvua mfululizo) Umeathiri shughuli za kilimo kuanzia katika maandalizi ya mashamba na upandaji hasa wa zao la mpunga kutokana na maeneo ya mashamba yaliyoandaliwa kujaa maji.
  • Upatikanaji hafifu wa pembejeo za kilimo hasa mbolea za kukuzia mazao.

  

3.1. Udhibiti wa Visumbufu vya Mazao

  • elimu imeendelea kutolewa namna ya utambuzi na udhibiti wa panya na viwavi jeshi vamizi.
  • Halmashauri imefanya jitihada za makusudi za kununua sumu ya kudhibiti panya(Zinc phoshide) kilo 50 pamoja na kilo 3 salio la msimu uliopita na kusambazwa kwa wakulima na kufanikiwa kuokoa ha.1073.5 za mazao ya nafaka zilizokuwa hatarini kuharibiwa.
  • Kwa kuwa tatizo bado linaendelea Halmashauri kwa fedha za ndani imeshanunua tena sumu kilo 200 kwa ajili ya kufanya kampeni ya kudhibiti panya katika vijiji vyote vilivyoathirika. Kazi hiyo inaweza kuanza rasmi ndani ya wiki hii.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa