• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

TANROADS YAKABIDHI MRADI WA UJENZI WA BARABARA YA MBINGU- CHITA KWA MKANDARASI TOKA CHINA

Posted on: June 26th, 2024

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Tarehe 25.06.2024 jioni, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekabidhi kwa Kampuni ya Uhandisi kutoka China, (China First Highway Engeneering Company) mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ijulikanayo kama Mbingu-Chita JKT.

Makabidhiano hayo yamefanywa na Mratibu wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya TANROADS mkoa wa Morogoro mhandisi Geofrey Mutakubwa akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba ndugu Jamary Idrisa, huko Mbingu.

Mhandisi Mutakubwa amesema ujenzi wa barabara ya Mbingu- Chita JKT yenye urefu wa kilomita 37.5 unatazamiwa kufanyika kwa kipindi cha miezi 20 kuanzia tarehe 25.06.2024 na fedha za utekelezaji wa mradi huo zimetolewa na Serikali ya Tanzania inayo ongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


“Mradi huu unagharimu shilingi bilioni 70.8 pesa ya Tanzania na pesa yote imetolewa na Serikali ya Tanzania pekee, hivyo watanzania na hasa wananchi wa Mlimba hatuna budi kuishukuru sana Serikali kwa jambo hili makini sana” alieleza Mutabuka.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba ndugu Jamary Idrisa amesema ujenzi wa barabara hiyo utakapo anza utaamsha ari ya wawekezaji kuja kuwekeza Mlimba hasa kwenye sekta ya kilimo ambayo ndio uti wa mgongo wa Halmashauri hiyo.

Pia, ndugu Jamary ameahidi kuwapa ushirikiano wa karibu wahandisi kutoka China wanaotekeleza mradi huo ili kuhakikisha wanaukamilisha kwa wakati.

Naye kiongozi wa timu ya wahandisi hao kutoka China amemshukuru Mkurugenzi Jamary kwa mapokezi mazuri na amempongeza kwa kuwa na Ofisi nzuri katika eneo lenye mandhari nzuri.

“Nimependa sana mazingira ya mahali hapa” alisema kiongozi huyo.

Kwa muda mrefu wananchi wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba wamekuwa wakiisihi Serikali kujenga barabara ya lami kwenye Halmashauri yao ili waondokane na adha ya usafiri hasa kipindi cha masika ambapo barabara zimekuwa zikiharibika sana na kusababisha wananchi kushindwa kutoka ama kuingia kwenye maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo.

Ni hakika kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Mbingu-Chita JKT kutaamsha furaha na tabasamu mioyoni mwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba kwani suala la kuwa na barabara nzuri na imara ni kiu na shauku yao ya muda mrefu.

MWISHO  

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa