• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

UANDIKISHAJI KWA WANAFUNZI ELIMU MSINGI 2018

Posted on: March 1st, 2018

Uandikishaji wa wanafunzi shule za msingi katika halmashauri ya wilaya ya Kilombero unaendelea na utafungwa rasmi ifikapo Machi 3 mwaka huu.

Kwa mujibu wa kaimu afisa elimu msingi katika halmashauri hii, Bi Zakia Fandey amesema kwa hadi kufikia Februari 23 mwaka huu wanafunzi wa darasa la awali walioandikishwa ni 10,879 sawa na asilimia 116 huku waliotazamiwa kuandikishwa walikuwa watoto  9357.

Bi Fandey amesema kuwa wanafunzi waliotazamiwa kuandishwa darasa la kwanza walikuwa 10,962 lakini hadi sasa walioandikishwa ni wanafunzi 11,640 sawa na asilimia 106.

Kwa upande wa mahitaji ya madarasa ya awali,Bi Fandey amesema halmashauri ina mahitaji ya madarasa 333 kwani yaliyopo hivi sasa ni madarasa 46 na upungufu ni madarasa 287 na kwa madarasa ya darasa la kwanza mahitaji ni madarasa 292 na yaliyopo 109 na upungufu madarasa 183.

Kaimu Afisa elimu huyo amesema mafanikio ya zoezi la uandikishaji limeleta changamoto mbalimbali zikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa kutokana na ongezeko la uandikishaji,upungufu wa madawati kutokana na ongezeko la uandikishaji na upungufu wa walimu wenye ujuzi wa kufundisha madarasa hayo.

Pia changamoto nyingine ni pamoja na jamii za wafugaji kuhama na watoto wao bila kufuata utaratibu na makazi ya wanafunzi kuwa mbali na shule hivyo baadgi ya watoto kutembea mwendo mrefu kufuata huduma.

Hata hivyo kaimu afisa elimu huyo amesema halmashauri imeendelea kutatua changamoto zinazokabili zoezi hili katika maeneo tajwa ikiwemo upungufu wa madawati kwa kutengeneza madawati kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza baada ya hapo itatengeneza madawati kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi ambapo mahitaji ni 1277 na kipaumbele kitazingatia maeneo yaliyoonesha ongezeko kubwa la uandikishaji na zoezi litaanza kwa kutengeneza madawati 422.

Kwa upande wa maboma halmashauri imejidhatiti kupeleka fedha kwa ajili ya kumalizia maboma yote yaliyo tayari kwa kupeleka vifaa vya kiwandani na upande wa walimu serikali inaendelea kuwajengea uwezo walimu wanaofundisha madarasa hayo kwa kuwapatia mafunzo chini ya mradi wa Tusome Pamoja.

Aidha halmashauri inaendelea kuelimisha jamii za kifugaji kuzingatia taratibu za uhamisho kwa watoto wao na pia kuendelea kuelimisha na kuhamasisha jamii kujitolea nguvu kazi kwa ajili ya ujenzi wa maboma kwa shule mpya ili watoto wasitembee mwendo mrefu kufuata huduma ya elimu.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa