• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Ukweli juu ya uvamizi wa shamba la mpira, Kilombero

Posted on: November 28th, 2018

Pichani juu: Mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo (Aliyeshika kipaza sauti) akiongea na wananchi.

Kutokana  na uongozi wa Shamba la mpira namba 165, kata ya Mwaya Wilaya ya Kilombero kuwaruhusu wananchi kufanya shughuli mbalimbali za kilimo na kibinaadamu, imepelekea kuibuka kwa mgogoro mkubwa baina ya Serikali ya wilaya ya Kilombero na wananchi hao, kwa kinachodaiwa kwamba alama za mipaka zilizopandwa na uongozi wa Shamba hilo mwaka 1978 wananchi hawakushirikishwa.

Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo, Awali shamba hilo lilikuwa ni msitu wa hifadhi ulioanzishwa na wakoloni, na ilipofika 1967 lilitangazwa kama misitu wa kalunga kwa tangazo la serikali la tarehe 08/12/1967, na kupewa namba 350, pia mwaka 1976 msitu huo ulipimwa na wizara ya maliasili na utalii nakupewa JB namba 638, katika mwaka 1980 serikali ilibadilisha matumizi ya msitu huo kutoka kwenye ardhi ya hifadhi na kuwa shamba kwa tangazo la serikali namba 114 la tarehe 01/08/198, na kukabidhiwa General Tyre Ltd, kwa matumizi ya upandaji wa miti ya mpira.

Ndg Ihunyo amesema kuwa zoezi la upimaji na umilikishaji wa shamba hilo, haukuhusisha viongozi wa kijiji vinavyopakana wala wananchi wa vijiji hivyo kama wanavyodai wananchi hao, kwakuwa ardhi hiyo haikuwa ardhi  ya kijiji, bali ilikuwa ni ardhi ya hifadhi ambayo ilikuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kumaliza mgogoro huo kwa kufanya jitihada kwa kuwahusisha viongozi wa vijiji vyote vinavyopakana na Shamba hilo kwa nyakati tofauti ili kupata muhafaka wa mgogoro huo, amesema Ndg Ihunyo.

Aidha matokeo ya vikao mbalimbali vilivyokuwa vikifanywa kati ya  tarehe 18 na 19 julai 2018 kwa kuwahusisha Maofisa/watumishi wa shamba hilo la mpira, yaliwezesha kufanya uhakiki upya wa shamba hilo,kwa kuwashirikisha baadhi ya wakulima ili kujiridhisha juu ya malalamiko kutoka kwa wananchi.

Ndg Ihunyo aliendelea kusema kuwa, kwa sasa kuna wavamizi wasiopungua 302, na kati ya hao ishirini ni wavamizi wa kilimo na makazi , na 269 wanalima kwa kibali kutoka katika uongozi wa shamba hilo, ambao wanadai maeneo hayo ni ya kwao huku wengi wakiwa na sababu kuwa, maeneo hayo wameyarithi kutoka kwa mababu zao, hivyo kuhalalisha kuwa ni maeneo ya kitu ambacho si kweli, sababu maeneo hayo, walipewa tu kulima ambapo serikali ingekuja kuyachukua muda wowote ule, sababu yalikwishatengwa kwaajili ya kilimo cha mpira na miti.

Sanjari na hayo Ndg Ihunyo amesema kuwa tayari kuna ulinzi mkali sana eneo hilo, na hatakiwi mtu yeyote Yule kufanya shughuli zozote za kimaendeleo eneo hilo, ili kuweza kuepusha migogoro zaidi inayoweza kutokea, sababu maeneo hayo yapo kisheria katika umiliki wa shirika la maendeleo ya taifa (NDC).

Hatahivyo kwa mujibu wa sheria zilizopo, yeyote atakayelima shamba hilo ni mvamizi ,na hii ni kutokana na  shamba hilo la mpira kupimwa na kuidhinishwa na Wizara ya ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi, na kumilikishwa (NDC).

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa