• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MGOGORO WA ARDHI KATI YA MALINYI NA KILOMBERO

Posted on: March 24th, 2017

WAKATI mvutano Wa kugombea kijiji cha Ngombo ukiendelea baina ya wilaya mbili za Kilombero NA Malinyi,wajumbe Wa kamati ya ushauri(DCC) Wilaya ya Kilombero kwa kauli moja wamesema mipaka inayotambulika kiserikali iheshimike kwa kijiji hicho kuonekana kipo Wilaya ya Kilombero.

Wakizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya,wajumbe hao walisema wanashangaa ofisi ya Mkuu Wa mkoa kuendelea kulikumbatia suala hilo wakati wakielewa katika ramani inaonyesha kuwa eneo la kijiji hicho lipo ndani ya Wilaya yao.

Akiwasilisha ajenda hiyo kwa wajumbe,mwenyekiti Wa kikao hicho ambae ni Mkuu Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo alisema kuwa ameagizwa NA ofisi ya Mkuu Wa mkoa kuanza kuchukua upya maoni Wa wajumbe Wa Wilaya ili wao wakikutana katika kikao cha Rcc wapokee maoni ya pande zote mbili kisha kutoa maamuzi.

Ihunyo alisema mwaka uliopita Mkuu Wa mkoa aliitisha kikao cha kamati ya ulinzi NA Usalama NA viongozi Wa Wilaya zote mbili ili kulijadili suala hilo lakini wajumbe Wa Wilaya ya Malinyi hawakutokea hivyo kuagiza wajumbe Wa DCC kulijadili suala hilo.

Hivyo aliwataka wajumbe kutoa ushauri ukizingatia kuwa mipaka toka Tamisema inaonyesha kabisa kuwa eneo hilo lipo ndani ya Wilaya ya Kilombero licha ya wananchi wake kupata Huduma muhimu wilaya ya Malinyi.

Katibu Wa chama cha mapinduzi(Ccm) Wilaya ya Kilombero Bakari Mfaume alisema kuwa kimsingi eneo lipo wilaya ya Kilombero  NA mamlaka za wilaya ya Kilombero zilichangia eneo hilo kuchukuliwa NA iliyokuwa wilaya ya Ulanga kabla ya kugawanywa NA kuwa wilaya mbili za Ulanga NA Malinyi .

Mfaume alitaja sababu zilizochangia eneo hilo kuchukuliwa ni kutopeleka Huduma za kijamii kwa muda mrefu NA hali hiyo ilipelekea wananchi Wa eneo hilo kujiona wapo wilaya ya Ulanga NA kupelekea kuwa NA Mtendaji NA mwenyekiti wanaotambulika wilaya mpya ya Malinyi .

Ameishauri serikali kupitia halmashauri ya wilaya ipeleke watendaji NA ikiwezekana uitishwe uchaguzi eneo hilo ili kweli wananchi wawe NA imani kuwa wilaya yao inawajali NA wakiruhusu eneo hilo liende Malinyi kuna hatari maeneo mengi yaliyopo pembezoni yatachukuliwa.

Naye mwenyekiti Wa Chama cha demokrasia NA Maendeleo(Chadema) wilaya ya Kilombero Shabani Mikongolo alisema mipaka iliyowekwa iheshimiwe NA kama wananchi wanahudumiwa wilaya ya Malinyi sio hoja NA kusema kuwa mbona watu Wa kata ya Uchindile ipo wilaya ya Kilombero lakini Huduma zote za kijamii wanazipata eneo la Mufindi lakini wao wanahesabika wapo Kilombero.

Mikongolo amewataka wajumbe Wa kikao cha ushauri cha mkoa(Rcc) ambacho kitaa hivi karibuni waheshimu mipaka inayotambulika NA watoe maamuzi haraka iwezekanavyo ili halmashauri ipeleke watendaji eneo hilo.

Mwisho....

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa