• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Wanafunzi wakumbwa na mapepo, DC atoa neno

Posted on: August 16th, 2018

Pichani juu: Mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo akizungumza na wakazi wa kijiji cha Msolwa

MKUU Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo amesitukua mtego aliowekewa na wakazi Wa kijjji cha Msolwa Stesheni waliotaka Mkuu huyo awaruhusu kuwakamata na kuwapeleka kwa mganga wale wote wanaohisiwa uchawi katika kijiji hicho.

Tukio hilo la aina yake limetokea Jana baada ya wakazi Wa kijiji hicho kupiga kura za siri za kuwabaini wachawi ambao wanahisiwa kusumbua wanafunzi  wa kike Wa shule ya msingi Kibong'oto kupatwa na mapepo na wanafunzi 24 wamekumbwa na mapepo na kuibua hali ya sintofahamu katika kijjji hicho.

Baada ya kutokea kwa mapepo hayo kwa wanafunzi ndipo ulipoitishwa mkutano Wa kijiji na wananchi kudai kuwa kuna wazee ambao ndio wanasumbua wanafunzi hao na kutaka kupiga kura za siri ili kuwataja na hatimae walipiga kura za siri za kuwataja.

Kilichofuata sasa ni kupewa kibali na kijiji ili wawakamate na kuwapeleka kwa mganga Wa jadi aitwae Bibi Kalembwana, ili kunyolewa na hatimae kutolewa uchawi, ingawa zoezi hilo lilishindikana kwa viongozi wa kijiji kuhofia kuvunjika kwa amani kijijini hapo hatimae kulifikisha suala hilo kwa Mkuu Wa Wilaya ili kulipatia ufumbuzi.

Akihutubia mamia ya wananchi waliokuwa na shauku ya kupata kibali kutoka kwa Mkuu huyo Wa wilaya,Ihunyo alipotoa nafasi ya kuwasikikiza wananchi kila Mwananchi aliyeinuka alimweleza Mkuu huyo wa wikaya kuwa njia pekee ya kuondoa tatizo kwa wanafunzi hao ni kuruhusu wahusika wakamatwe na kisha kupelekwa kwa bibi kunyolewa na ndipo tatizo hilo litamalizika kijijini hapo.

Naye Mwenyekiti Wa halmashauri ya Wilaya ya Kilombero David Ligazio, aliwasihi wananchi hao kuwa tatizo hilo wanaweza kulimaliza wenyewe bila kupelekana kwa bibi, hivyo kuwaomba wanaofanya kitendo hicho kuwaonea huruma watoto hao, na kama hali ikiendelea hivyo kuna hatari shule kufungwa na watoto kukosa masomo.

Licha ya maelekezo kutoka kwa viongozi Wa wilaya na Wa dini asilimia kubwa ya wananchi walitaka wahusika wakamatwe na kupelekwa kwa bibi, kwani wanajulikana na kutamba kuwa hamna MTU ataewafanya lolote na atakaejipendekeza kwao nae watamdhuru.

Baada ya kusikiliza maelezo ya pande zote ndipo Ihunyo alipotoa maamuzi kuwa, serikali haitaruhusu mtu yeyote kukamatwa na kupelekwa kwa bibi kunyolewa kwa kisingizio cha uchawi na yeyote atakaethubutu hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Ihunyo alisema, serikali haitambui uchawi na kama suala hilo likiruhusiwa litaleta madhara katika kijiji hivyo kuwaomba wazee na viongozi Wa dini wasaidie ili matatizo hayo yaishe.

Awali akitoa taarifa ya tatizo la mapepo kwa wanafunzi Wa kike shuleni hapo, Afisa Mtendaji Wa kata ya Msolwa Stesheni Joachim Lyembela alisema, lilianza kwa mwanafunzi mmoja Wa darasa LA saba akiwa kwenye mtihani Wa kujipima Wa kata hapo Machi mwaka huu.

Lyembela alisema Juni mwaka huu tatizo liliendelea na kadri siku zinasonga tatizo hilo kuongezeka na wanafunzi wanaokumbwa na mapepo ni Wa kike kuanzia darasa la nne hadi la saba na hali hiyo imepelekea shuleni hapo kukosekana amani na walimu kushindwa kufundisha kwa wiki tatu sasa.

Mtendaji huyo amebainisha kuwa wanafunzi wanaotokewa na mapepo, wamekuwa wakiingia ofisini na kufanya vurugu na kuwakaba wanafunzi wengine, na kufanya wanafunzi wengine kuogopa kufika shuleni na hadi sasa wanafunzi 24 wametokewa na mapepo na wengine zaidi ya 30 huwatokea siku moja moja kutoka madarasa tofauti.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa