• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

ZIARA YA KITENGO CHA UTAMADUNI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO

Posted on: March 5th, 2018

Picha ya hapo juu inaonyesha sehemu ya Tambiko ya Chifu wa Utengule

SEHEMU YA KWANZA.

Mabaki ya gari alilokuwa akitumia chifu Kiwanga

Ofisi ya utamaduni ilipata fursa ya kuzifikia kata sita ili kujifunza na kukusanya habari za kihistoria  na kitalii za wilaya ya kilombero ambazo taarifa zake za awali ziliifikia ofisi kupitia watendaji kata.

Kata zilizotembelewa ni Utengule,Mlimba,Chisano,Chita Mchombe na Mbingu.Katika kata za Mlimba,Chita ,Mchombe na Mbingu walialikwa wadau wa Utamaduni wa kata za jirani ili kupata nafasi za kujadiliana juu ya maendeleo ya sekta ndani ya Halmashauri ya Kilombero.

KATA ZILIZOJITOKEZA

KATA YA UTENGULE

Kuna taarifa za Utawala wa Chifu Kiwanga ambao bado unaenziwa  hadi hivi sasa.

Chifu aliyeonwa alijitambulisha kwa jina la Chifu Soliambingu wa pili.Chifu huyo aliupokea Uchifu kutoka kwa ChifuTowegale wa pili tangu 2008.

Chifu aliwabainisha machifu waliomtangulia kwa kufuatana kama ifuatavyo; Chifu Manga,Chifu Kihegula,Chifu Luvatu,Chifu Mgovano,Chifu Ndivale,Chifu Msavila,Chifu Mtengela,Chifu Kiwanga wa Kwanza ambaye Utawala wake Uliishia 1905,Chifu Kiwanga wa Pili ,Chifu Soliambibgu wa Kwanza,ChifuTowegale wa kwanza,Chifu Towegale wa pili na Mwisho Chifu Soliambingu ambaye anaendeleza Utawala huo hadi sasa kuanzia mwaka 2008.

ENEO LA MAKAZI YA CHIFU KIWANGA

Katika makao makuu ya Utawala wa chifu Kiwanga ambapo palijulikana kama IGOMBE yaani ikulu ya chifu yameonekana  majengo kadhaa ambayo kwa sasa ni magofu  nayo ni jengo la Mahakama ya Utawala wa kichifu ,Mabaki ya Gari alilotumia chifu,Mnara wa nyumba ya tambiko,shule,na nyumba ya Utawala yaani Ikulu.

Mabaki ya iliyokuwa ikulu ya chifu Kiwanga

Chifu Soliambingu wa pili alitueleza kuwa,  enzi za Utawala wa chifu Towegale zilikuwa miaka ya 1920-1961,Chifu Towegale wa pili 1961-2008 na chifu Soliambingu wa pili 2008 hadi sasa.

Chifu alibainisha ngoma zilizokuwa maarufu enzi  zao zilikuwa, Luheyo,Lipala,Liketo na Mdulange. Chifu alisema akipewa nguvu ya kufufua ngoma hizo yuko tayari kwani bado ana uwezo wa kuzifundisha.Nguvu aliyoisema ni pamoja na Gharama za Maleba,Ngoma,Vifaa vingine vya kukamilisha ngoma,gharama za mafunzo kwa vijana na wazee, uandaaji matamashana Recording.

Chifu aliongeza kuwa Katika enzi za utawala wake kulikuwa na bwawa maarufu lililojulikana kama Ngapemba ambapo wakati wote lilikuwa na maji mengi na kutoa samaki kwa wingi kukidhi jamii yao.Bwawa hilo kwa sasa limepoteza umaarufu wake kutokana na ukiukwaji wa baadhi ya miiko ya matumizi ya bwawa hilo

Chifu aliongeza kuwa usafiri maarufu wa machifu ulikuwa ni mitumbwi 3  ya usafiri wa majini na Gari la  kifahari  kwa ajili ya nchi kavu. Katika safari alieleza kuwa chifu alikuwa akisafiri na wake zake kati ya 60 na 70.

Mwisho chifu aliomba uhisani serikalini kwa ajili ya kukarabati majengo ya utawala huo ili kutunza historia ya utawala ingawaje kwa sasa hauna majukumu mazito kama enzi zake. Aidha aliomba uwepo utaratibu wa historia hiyo kufundishwa mashuleni hii ni pamoja na mila,desturi nzuri na ngoma za asili.

Je unataka kujua habari juu ya chura wanaozaa? Endelea kutembelea website yetu kwaajili ya sehemu ya pili ya maelezo haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA MNADA December 16, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2023 December 14, 2022
  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA MATUMIZI YA KAWAIDA JULAI 2022 August 01, 2022
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA IMEPOKEA PESA ZA MATUMIZI YA KAWAIDA KUTOKA HAZINA (OC) KWA MWEZI NOVEMBA 2022 TSHS 35,294,000/= December 05, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAPOKEZI YA FEDHA ZA OC KWA MWEZI JANUARY TSH. 189,174.000/=

    February 07, 2023
  • MHE. DUNSTAN KYOBYA MKUU WA WILAYA YA KILOMBERO ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI NAKAGURU

    February 02, 2023
  • MHE. DUNSTAN KYOBYA MKUU WA WILAYA YA KILOMBERO ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI NAKAGURU

    February 02, 2023
  • WAZAZI WASIOPELEKA WATOTO SHULE KUCHUKULIWA HATUA

    January 23, 2023
  • Angalia zote

Video

MHE. WAKILI DUNSTANI KYOBYA AHAIDI TSH. 500,000.00/= KWA KILA MWANAFUNZI ATAKAYEPATA DIVISHENI 1.7.
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • Tovuti kuu ya Takwimu huria

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa