• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MKUU WA MKOA WA MOROGORO Dk STEVEN KABWE AKIZUNGUMZA NA WARATIBU ELIMU KATA PAMOJA NA WAKUU WA SHULE WILAYANI KILOMBERO

Posted on: January 23rd, 2018

Mkuu Wa mkoa Wa Morogoro Dk Steven Kebwe amekerwa na idadi kubwa ya wanafunzi Wa sekondari wilayani Kilombero kukatishwa masomo yao baada ya kupewa mimba huku akitoa onyo kwa Hakimu yeyote anaecheza na kesi za mimba kwa wanafunzi atakula nae Sahani moja.

Kauli hiyo ameitoa jana mjini Ifakara baada ya kufanya kikao cha pamoja baina yake na wakuu Wa shule na waratibu elimu kata Wa Wilaya ya Kilombero katika shule ya sekondari Ifakara chenye lengo la kupata taarifa za usimamizi Wa elimu katika Wilaya hiyo.

Katika taarifa za hali ya elimu katika halmashauri Mbili za Kilombero na Mji Ifakara ilionyesha kuwa wanafunzi 63 Wa sekondari walipata mimba hivyo kuacha masomo yao kwa mwaka 2017.

Dk Kebwe alisema idadi hiyo ni kubwa hivyo amemuagiza Mkuu Wa Wilaya kuhakikisha kwamba wale wote waliohusika na kuwapa wanafunzi hao ujauzito wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria haraka iwezekanavyo.

Mkuu huyo Wa mkoa pia ametoa onyo kwa Hakimu yeyote atakaecheza na kesi ya mimba kwa mwanafunzi atamshughulikia sababu wapo baadhi yao wanacheza na wazazi Wa watoto ama wahusika na kupindisha Ukweli ama kuchelewesha ushahidi.

Amezitaka Mahakama kuharakisha kesi zote zinazohusu ujauzito kwa wanafunzi na mahakimu wasilete kisingizio cha ushahidi wakati inaonyesha kabisa wanafunzi hao walirubuniwa kwa umri wao Mdogo ama tamaa na wahusika wapo humohumo mitaani.

Kuhusu utekelezaji Wa agizo LA Rais MAgufuli LA kutaka wazazi kutochangia michango mashuleni,Mkuu huyo Wa mkoa alisema kama mkoa ameunda kamati maalum ya kufuatilia walimu wanaochangisha wazazi na kubainisha kuwa Kamati hiyo itajumuisha watu watano kutoka mkoani na pia Wilaya zote na ameipa siku 14 kumpelekea taarifa mezani kwake.

Alisema walimu wakuu na wakuu wa shule wahakikishe wanafuata utaratibu kama ambavyo unafafanuliwa vizuri katika waraka Wa sita Wa mwaka 2016 na wazazi ama walezi wasipewe mzigo Wa michango na pale amvapo wanakubaliana kwa Uhuru wao bila shinikizo ruksa kuchangia lakini bila shuruti.

Kwa mujibu Wa Mkuu huyo Wa mkoa kuwa kila mwezi kwa sasa mkoa unapewa kiasi cha shilingi bilioni 1.3 toka serikali kuu kwa ajili ya kutekeleza Sera ya elimu bila malipo na kusema kuwa atashangaa walimu ama kamati za shule zikiendelea kunga'ang'ania kuwachangisha wazazi wakati Fedha zinafika mashuleni kwa wakati ili kutekeleza Sera hiyo.

Kwa upande wake Afisa elimu mkoa Wa morogoro  Euphransia Bubhuma alisema kwa mwaka 2017 hali ya ufaulu ilipanda toka nafasi ya 27 mwaja 2016 hadi nafasi ya 11 kitaifa mwaka jana kwa matokeo ya darasa LA saba na darasa LA nne walitoka nafasi ya  15 mwaka juzi hadi nafasi ya 11 mwaka jana.

Bubhuma alitaja mkakati Wa mkoa katika kuinua kiwango cha taaluma ni pamoja na kusimamia mahudhurio ya wanafunzi darasani sambamba na kusimamia ufundishaji Wa dhati kwa walimu darasani na utoaji Wa chakula kwa wanafunzi ili kuwajengea uwezo darasani.

Kuhusu changamoto za mimba mashuleni alisema warahakikisha wale wote watakaohusika wachukuliwe hatua za kisheria na walimu watoe elimu ya kijinsia kwa wanafunzi Wa kike ili kumaliza tatizo hili.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA DEREVA NA MWENDESHA OFISI MLIMBA DC July 01, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa