• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

Posted on: January 18th, 2026


Halmashauri ya Wilaya Mlimba imefanya Mkutano wa Robo ya Pili wa Baraza la Madiwani, kwa lengo la kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za Halmashauri kutoka kwa kamati za kudumu za Halmashauri, pamoja na TARURA na RUWASA.

Akiongoza Mkutano huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, Mhe. Martha Mkula, amewasisitiza wajumbe kuhamasisha wananchi kulipa ushuru kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato ya halmashauri, ili kuongeza mapato na kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri.

Mhe. Mkula pia ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha Robo ya Pili, huku akiwataka TARURA kuongeza kasi katika ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ili ziweze kupitika kwa wakati wote.

Kupitia mkutano huo, mwakilishi wa Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilombero, Acrey Lawika, amesema miradi mikubwa ya maji, ikiwemo Mbingu, Igima na Mlimba, imekamilika kwa asilimia 90, na wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama. 

Amefafanua kuwa Ofisi ya RUWASA Kilombero tayari imekamilisha mradi wa uchimbaji wa visima vitano, virefu, vya Samia katika vijiji mbalimbali ikiwemo Mkuyuni, Miwangani na Lumumwe, na mpango wa sasa wa Ofisi hiyo ni kuchimba visima vingine vitano katika vijiji vipya ikiwemo Msita na Njage, pamoja na kupanua mradi wa kisima cha Uchindile Lugala.

Kwa upande wake, Meneja wa TARURA Kilombero, Mhandisi Fidelis Kessy, ameliambia Baraza la Madiwani kwamba, katika Halmashauri ya Mlimba, madaraja makubwa matatu na barabara zenye jumla ya kilomita 1,060, zinajengwa na kuimarishwa kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha kama vile Road Fund, Tozo ya Mafuta, Jimbo la Mlimba na Benki ya Dunia. 

Madaraja makubwa yanayojengwa kwa fedha za Benki ya Dunia ni daraja la Mbasa katika kata ya Mchombe, Isago katika kata ya Mngeta na Matete katika kata ya Mbingu. 

Aidha, TARURA inaendelea na ujenzi wa barabara za changarawe na lami, pamoja na makaravati na madaraja katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ili kuhakikisha barabara zinapitika kwa wakati wote.

Baraza la Madiwani limepongeza juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuimarisha huduma kwa jamii, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara na upelekaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi.

Mkutano huo umehudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani kutoka kata 16 za Halmashauri, viongozi wa vyama vya siasa ikiwemo Katibu wa Chama cha Mapinduzi, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero pamoja na Kamati ya Usalama ya Wilaya.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEAZIMIA KUHIMIZA UPATIKANAJI WA LISHE SHULENI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA KUGAWA BURE VYANDARUA VYENYE DAWA

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa

  • HUSKYSLOT
  • ROBOSLOT
  • TAHUPLAY
  • AWPSLOT
  • DANATOTO
  • Situs Toto