• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

Posted on: January 18th, 2026


Mradi wa Mifumo ya Chakula, Matumizi ya Ardhi na Urejeshaji wa Uoto wa Asili (FOLUR) umeingia rasmi hatua ya utekelezaji kwa vitendo, baada ya Sekretarieti ya mradi huo kukutana Man’gula–Ifakara Januari 15–17, 2026, kwa lengo la kuunganisha mipango ya usimamizi wa shughuli za kisekta za kilimo, ardhi, misitu, wanyamapori na maji, ili kuwa na mpango jumuishi wa utekelezaji wa shughuli za mradi katika maeneo ya mradi ambayo ni Halmashauri ya Wilaya Mlimba na Halmashauri za Kaskazini A na B-Unguja.

Hatua hiyo inaashiria kuanza kwa mwaka wa pili wa utekelezaji wa Mradi wa FOLUR Tanzania, unaofadhiliwa na Mfuko wa Dunia wa Uhifadhi wa Mazingira (GEF), na kutekelezwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mratibu wa Mradi katika Halmashauri ya Wilaya Mlimba, Ndg. Joseph Mgana, alisema kuwa hatua ya kuanza utekelezaji wa vitendo imefikiwa baada ya kukamilika kwa maandalizi yote ya awali ya mradi.

Alisema maandalizi hayo yalijumuisha kuanzishwa kwa ofisi ya mradi, kuutambulisha mradi kwa menejimenti za halmashauri husika, pamoja na kwa wananchi wa vijiji vinavyotarajiwa kunufaika na mradi kote Tanzania Bara na Zanzibar.

“Katika mwaka wa kwanza wa mradi, tumepokea na kujadili matokeo ya tafiti za kisekta kutoka kwa wadau wa serikali na binafsi, wakiwemo washauri elekezi na watekelezaji wenza. Matokeo hayo yametumika kuandaa mipango kazi ya kisekta, ambayo sasa tunaenda kuitekeleza kwa pamoja,” alisema Ndg. Mgana.

Aliongeza kuwa baada ya kukamilika kwa hatua hiyo ya maandalizi, mradi sasa unaanza utekelezaji jumuishi katika vijiji vyote 49 vya mradi vilivyopo Tanzania Bara na Zanzibar.

Kwa upande wake, Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa FOLUR kutoka Wizara Simamizi ya Mradi, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ndg. Wanjala Mgaywa, alisema kuwa FOLUR ni mradi wa kwanza wa kitaifa unaolenga kuimarisha uhifadhi wa rasilimali maji, ardhi na misitu kwa mtazamo wa pamoja, huku kilimo endelevu cha zao la mpunga kikiwa ni eneo mahsusi la utekelezaji.

“Tunaamini kuwa ili mpunga ulimwe kwa tija na kwa uendelevu, ni lazima tuhifadhi misitu ambayo ndiyo chanzo kikuu cha maji. Aidha, ni muhimu kuweka utaratibu wa matumizi bora ya maji, pamoja na kupanga matumizi ya ardhi ili mkulima alime katika eneo dogo lakini azalishe kwa wingi,” alisema Ndg. Mgaywa.

Alifafanua kuwa kupitia mradi wa FOLUR, wakulima watasaidiwa kupanga na kutumia ardhi yao kwa tija, huku juhudi za uhifadhi wa misitu zikichangia uzalishaji wa hewa ya kaboni itakayokuwa na manufaa ya kiuchumi kwa halmashauri za mradi na taifa kwa ujumla.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, jumla ya vijiji 23 kutoka kata za Mngeta, Mchombe, Mofu, Chin’anda, na Chisano vinatarajiwa kunufaika na mradi wa FOLUR. Vijiji hivyo ni Mofu, Kalenga, Ikwambi, Ihenga, Miyomboni, Mkusi, Njage, Mchombe, Nakaguru, Ijia na Lukolongo. 

Vingine ni Mngeta, Kidete, Isago, Mkangawalo,Luvilikila, Ikule, Itongowa, Chin’ganda, Lufulu, Udagaji, Chisano na Mgugwe.

Mradi wa FOLUR unalenga kuchangia katika kuimarisha mifumo endelevu ya uzalishaji wa chakula, kuhifadhi rasilimali asilia na kuboresha maisha ya wananchi katika maeneo ya mradi kupitia mbinu jumuishi za usimamizi wa ardhi na mazingira.

MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEAZIMIA KUHIMIZA UPATIKANAJI WA LISHE SHULENI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA KUGAWA BURE VYANDARUA VYENYE DAWA

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa

  • HUSKYSLOT
  • ROBOSLOT
  • TAHUPLAY
  • AWPSLOT
  • DANATOTO
  • Situs Toto