Mkuu wa wilaya ya Kilombero Ndg James Ihunyo, ameendelea kusimamia vyema sana ujenzi wa Mahakama ya Kilombero, kwa kuhakikisha kuwa jengo hilo linajengwa haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa agizo la Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli.
Akizungumza na mwandishi wa Habari hii Ndg Ihunyo amekumbusha kuwa ujenzi wa Mahakama hiyo umetokana na maombi ya Ndugu Ismail Limbenga aliyomuomba Mhe. Magufuli kusaidia kuezeka mahakama hiyo kwani wananchi wa eneo hilo wanapata tabu sana kupata huduma hizo za kimahakama.
Aidha Ndg Ihunyo amesema kuwa kutokana na tathmini ya wataalam iligundulika kuwa jengo hilo si salama kwa matumizi, hivyo halikuhitaji tu kuezekwa bali kujengwa upya, hivyo alianza kufanya harakati za kupatikana kwa pesa ambazo zimeweza kujenga jengo hilo katika hali ya kisasa hadi kufikia kiwango cha kusubiri kumwagwa linta na kisha kuezekwa kama alivyoagiza Mhe. Rais.
Katika hatua nyingine, Ndg Ihunyo aliwashukuru wadau mbalimbali waliojitolea kufanikisha ujenzi huo, wakiwemo ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero ambayo imechangia vifaa mbalimbali vya ujenzi na kulipa mafundi waliojenga jengo hilo, serikali ya vijiji vitatu vinavyounda kata ya Kiberege, waliochangia matofali zaidi ya Alfu saba, uongozi wa kiwanda cha sukari Kilombero ambacho kimechangia vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni thelathini, diwani wa Kiberege aliyetoa matofali mia tano, mtendaji mkuu wa mahakama aliyetoa zadi ya miliomi tano, shule ya msingi Kiberege iliyotoa mbao kwaajili ya kuezekea pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya iliyochangia mifuko ya simenti mia moja pamoja na nondo 23.
Pamoja na yote hayo Ndg Ihunyo amesema kuwa kwa namna ya kipekee anamshukuru sana Mhe. Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania aliyetoa jumla ya shilingi milioni tano na kutoa agizo la ujenzi wa mahakama hiyo pamoja na kuahidi kuisimamia ili ijengwe kama kama anavyotaka, kwani bila ya yeye, mahakama hiyo isingejengwa kwa kipindi hiki.
Pia ndg Ihunyo aliwaomba wananchi kuchangia kwenye kata nyingine ili kuhakikisha kuwa, na kwenye kata hizo kunajengwa mahakama nyingine ambazo zitawasaidia watu kupata huduma hizo, kuliko kwenda maeneo ya mbali kufata huduma hiyo kwa kutumia gharama
Mngeta Kijiji cha Itongoa
Anuani: P.O.BOX 263
Simu: 023 293 1523
Mobile: 0232931523
Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz
Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa