• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

DC KYOBYA AWATAKA WANANCHI MLIMBA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA MPOX

Posted on: August 27th, 2024

Na, Milka Kaswamila-Mlimba DC

Tarehe 22.08.2024, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero mhe. Dunstan Kyobya aliongoza Kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi Wilaya, kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba Itongowa-Mngeta.

Katika kikao hicho mhe. Kyobya ametoa maagizo kadhaa kwa Halmashauri ikiwemo kuhakikisha kasi ya utoaji huduma za chanjo inaongezeka, elimu kuhusu huduma ya usafiri wa dharura kwa wajawazito na watoto wachanga (M-mama) inatolewa kwa wananchi katika maeneo yote ya Halmashauri na wananchi kuhakikisha wanachukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa homa itokanayo na nyani (Mpox).

Mhe. Kyobya ametumia kikao hicho kutoa maagizo mengine ya jumla ikiwemo Ofisi ya Mkurugenzi kuhakikisha huduma ya umeme inafika mara moja kwenye Vituo vya Afya vya Uchindile na Igima, Zahanati zote zisizo na umeme zifanyiwe utaratibu wa kupelekewa huduma hiyo, miradi ya maendeleo iendelee kusimamiwa ili ikamilike kwa wakati na wananchi waendelee kujiandaa kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Kwa upande mwingine, mhe. Kyobya katika kikao hicho aligawa vitendea kazi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan (gwanda 37 na vishkwambi 35) kwa maafisa ugani 35 kutoka Kata zote za Halmashauri, ikiwa ni sehemu ya kutambua huduma yao kwa jamii na kuendelea kuimarisha mazingira yao ya kazi.

Wataalamu wa afya wa Halmashauri ya Mlimba waliwasilisha mada mbalimbali katika kikao hicho ikiwemo mada za huduma za mama na mtoto, M-mama, homa itokanayo na nyani (Mpox) na huduma za chanjo.

Aidha, kupitia kikao hicho, wananchi wamepaswa kufahamu kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa huduma ya usafiri wa dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga ambao hupata changamoto baada ya kujifungua, ambazo zinaweza kupelekea kifo.

Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Mlimba Dkt. Willy Kopela, huduma ya M-Mama inapatikana kwenye maeneo yote ndani ya Halmashauri kwa kupiga simu namba 115 bure.

Kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi Wilaya hufanyika mara mbili kwa mwaka yaani Januari-Juni na Julai-Desemba na kuhudhuriwa na viongozi wa makundi mbalimbali ikiwemo viongozi wa Dini, Vyama vya Siasa na Wazee.

MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa