• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEAZIMIA KUHIMIZA UPATIKANAJI WA LISHE SHULENI

Posted on: January 18th, 2026


Halmashauri ya Wilaya Mlimba imeazimia kuhimiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanapata milo miwili shuleni, ikiwa ni pamoja na uji wenye virutubisho wakati wa asubuhi na chakula cha mchana kinachozingatia mlo kamili.

Vilevile, halmashauri imeazimia kutoa elimu ya virutubisho kwa wakuu wa shule ili waweze kuhimiza wanafunzi kunywa uji na ugali wenye virutubisho na kuacha mazoea ya kula wali pekee.

Maazimio hayo yamekuja baada ya wasilisho la taarifa ya utekelezaji wa Afua za Lishe, lililofanywa na Afisa Lishe wa Halmashauri, Ndg. Bodygadi Buhari, katika Kikao cha Tathmini ya Lishe kwa Kipindi cha Julai–Desemba, kilichofanyika Jumamosi tarehe 17 Januari 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, kikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba, Mhe. Martha Mkula, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Wakili Dunstan Kyobya.

Kupitia taarifa hiyo, wajumbe walipongeza juhudi za Halmashauri kununua mashine tano za kuongeza virutubisho kwenye unga wa mahindi, ambazo tayari zimesambazwa katika kata tano zenye wamiliki wa mashine hizo. Wajumbe walisema mashine hizo zitasaidia kuimarisha Lishe bora kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Pia, wajumbe walihimiza usimamizi makini wa vyakula shuleni ili kuhakikisha vinajumuisha makundi yote saba ya chakula na kuimarisha afya ya mwili na akili za wanafunzi. 

Aidha, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Martha Mkula amewataka wazazi na walezi kuelewa kwamba kuchangia chakula cha mtoto shuleni si hiari bali ni wajibu, huku akisisitiza kuwa mahindi ni lazima yawepo ili kusaidia upatikanaji wa uji na ugali wenye virutubisho.

Kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Lishe Buhari, utekelezaji wa Afua za Lishe katika Halmashauri ya Mlimba unafanyika kwa mafanikio makubwa, kwani hakuna alama nyekundu zilizorekodiwa katika afua zote za lishe kwa wajawazito, watoto chini ya miaka mitano, na upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.

Katika kikao hicho, Mratibu wa Huduma za Bima wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, Dkt. Amani Nkilingi, pia aliwajengea uelewa wajumbe kuhusu Bima ya Afya kwa Wote, ambapo alisema kuwa mpango huo ni kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita, ukiendana na Dira ya Taifa 2050, Malengo Endelevu ya Milenia 2030, na Ilani ya CCM 2025–2030.

Dkt. Nkilingi alifafanua kuwa lengo ni kuondoa matabaka kwenye matibabu na kwamba Serikali itagharamia bima kwa makundi maalumu ambayo ni wazee, watoto, wajawazito na wenye ulemavu. 

Aidha, wananchi wengine watajiunga kwa hiari kwa gharama ya Sh. 150,000 kwa kaya isiyozidi watu sita, ambapo jumla ya huduma 372 zitatolewa ikiwemo huduma za kibingwa, uchunguzi, maabara, radiolojia, dawa na vifaa tiba. Aidha, bima ya Afya kwa Wote haitasababisha kuachishwa kwa bima nyingine kama NHIF, isipokuwa Bima ya CHIF tu itasimamishwa pale itakapokoma muda wake.

Kikao cha Tathmini ya Lishe kwa Kipindi cha Julai-Desemba cha Halmashauri ya Mlimba kilihudhuriwa na wadau mbalimbali, ikiwemo Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba, watendaji wa kata, na wakuu wa idara na vitengo vya Halmashauri.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEAZIMIA KUHIMIZA UPATIKANAJI WA LISHE SHULENI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA KUGAWA BURE VYANDARUA VYENYE DAWA

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa

  • HUSKYSLOT
  • ROBOSLOT
  • TAHUPLAY
  • AWPSLOT
  • DANATOTO
  • Situs Toto