• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA KUGAWA BURE VYANDARUA VYENYE DAWA

Posted on: January 18th, 2026


Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba imeanza maandalizi ya zoezi la ugawaji bure wa vyandarua vyenye dawa kwa kaya zake zote, kufuatia ujio wa wataalamu kutoka Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria, waliowasili halmashaurini hapo tarehe 16 Januari, 2026 kwa lengo la kutambulisha mpango huo wa Serikali.

Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la upokeaji wa Taarifa ya Utekelezaji wa Shughuli za Halmashauri kwa Kipindi cha Robo ya Pili (Oktoba–Desemba), uliofanyika tarehe 17 Januari, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Dkt. Christina Guveti, amesema kuwa jumla ya vyandarua 174,769 vinatarajiwa kusambazwa kwa wananchi wa halmashauri hiyo.

Dkt. Guveti amesema kuwa ugawaji huo utafanyika kwa utaratibu wa chandarua kimoja kwa kila wanakaya wawili, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kudhibiti na kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria.

Ametoa wito kwa Waheshimiwa Madiwani kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la utambuzi wa kaya, litakalofanyika kwa muda wa majuma mawili kuanzia Jumatatu tarehe 19 Januari, 2026, katika kaya zote, kambi za jeshi pamoja na shule za sekondari zilizopo ndani ya halmashauri.

Aidha, amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji kusimamia zoezi hilo kwa haki na uwazi, ili kuhakikisha kaya zote zinanufaika na ugawaji wa vyandarua hivyo, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha huduma muhimu za afya zinawafikia wananchi wote.

Dkt. Guveti ameongeza kuwa zoezi la ugawaji wa vyandarua vyenye dawa linasimamiwa na Bohari Kuu ya Dawa (MSD), baada ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia sekta ya afya kufanya utafiti uliobaini kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba ni miongoni mwa halmashauri saba kati ya tisa za Mkoa wa Morogoro zenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa wa malaria.

Amefafanua kuwa, kutokana na jiografia ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, vyandarua hivyo vitasambazwa katika vitongoji vyote ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma hiyo kwa usawa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba, Mhe. Martha Mkula, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha zoezi la ugawaji wa vyandarua hivyo, sambamba na utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya matumizi sahihi ya vyandarua, hatua itakayochangia kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria halmashaurini humo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA MWAKA 2025 November 05, 2025
  • MATOKEO YA USAILI WA MAANDISHI WA MAAFISA UGANI KWA AJILI YA MRADI WA MIFUMO YA CHAKULA, MARUMIZI YA ARDHI NA UREJESHAJI WA MAZINGIRA (FOLUR) KATIKA HALMASHAURI YA MLIMBA December 06, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA FOLUR KUANZA KUTEKELEZWA KWA VITENDO

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI, WA BARAZA LA MADIWANI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA IMEAZIMIA KUHIMIZA UPATIKANAJI WA LISHE SHULENI

    January 18, 2026
  • HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA KUGAWA BURE VYANDARUA VYENYE DAWA

    January 18, 2026
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa

  • HUSKYSLOT
  • ROBOSLOT
  • TAHUPLAY
  • AWPSLOT
  • DANATOTO
  • Situs Toto