• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Halmashauri ya wilaya ya Mlimba yakadiria bajeti yake

Posted on: January 25th, 2021

HALMASHAURI ya wilaya ya Mlimba inakadiria kupata jumla ya shilingi bilioni 33,805,381,339.19 kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Hayo yamebainishwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Mhandisi Stephano Kaliwa wakati wa mkutano maalum wa bajeti wa baraza la madiwani uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita makao makuu ya halmashauri hiyo Mngeta.

Mhandisi Kaliwa amesema bajeti hiyo imezingatia maeneo mahsusi na ya kipaumbele yaliyoainishwa katika mpango mkakati wa halmashauri wa mwaka 2016/2017-2021/2022,mwongozo wa uandaaji wa bajeti wa mwaka wa fedha wa 2021/2022 na mpango wa maendeleo wa taifa wa miaka mitano 2016/2017-2020/2021(FYDP II).

“Maeneo mengine yaliyozingatiwa katika bajeti ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa Ccm ya mwaka 2020/2025,sheria ya bajeti sura 439 pamoja na kanuni zake,mkakati wa taifa dhidi ya rushwa awamu ya tatu,malengo endelevu ya maendeleo na mwongozo wa ushirikiano wa kimaendeleo,”alisema.

Mkurugenzi huyo mtendaji ameyataja maeneo yaliyopewa kipaumbele katika sekta ya kilimo kuwa ni ununuzi wa mbegu za korosho kilogramu 1000 na kuandaa maandiko ya miradi ya umwagiliaji Udagaji na Kisegese na upande upande wa mifugo ni kutoa huduma ya chanjo mbalimbali kwa mifugo sambamba na kuboresha huduma ya uogeshaji kwa kujenga josho moja katika kijiji cha Namwawala.

Ameyataja maeneo mengine yaliyopewa kipaumbele ni katika sekta ya elimu ya msingi na sekondari kwa ukamilishaji wa maboma ya madarasa na nyumba za walimu,kuwapa kipaumbele walimu wanaoishi shule za  pembezoni na kukagua ubora wa elimu mara kwa mara katika shule za serikali na binafsi.

“Kwa upande wa sekta ya Afya tumepanga kuendeleza ujenzi wa kituo cha Afya Chita na kuanza ujenzi wa kituo cha Afya Igima na upande wa maji tumepanga kuboresha huduma za maji katika taasisi za umma kama shule na vituo vya afya kwenye shule za msingi 52,sekondari 10 na vituo vya afya 21”alisema.

Mhandisi Kaliwa amesema pia wanataraji kuboresha ukusanyaji wa mapato ya halmashauri ili kufikia malengo ya makusanyo kwa kutumia sheria ndogo na usimamizi mzuri wa matumizi na kutoa mikopo kiasi cha shilingi milioni 275 kwa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu.

Akielezea ukusanya wa mapato ya ndani,Mhandisi Kaliwa amesema jumla ya shilingi bilioni 2,750,000,000 wanakadiria kukusanya kutoka vyanzo vyake vya ndani kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

“Makadiro ya mapato hayo yanalengwa kutoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo ushuru wa mchele na mazao mengine,ushuru wa nyumba za kulala wageni,ushuru wa huduma,ushuru wa kuzoa taka,ukodishaji wa mali za halmashauri,ada ya kuuza kiwanja na leseni za biashara,”alibainisha.

Vyanzo vingine ni pamoja na vibali vya burudani,ushuru wa mazao ya misitu,ushuru wa vibanda vya soko,huduma za ardhi,ada za mifugo,ushuru wa machinjio,ushuru wa samaki,leseni za uvuvi,ada za leseni za vyombo vya uvuvi na faini mbalimbali.

Hata hivyo mkurugenzi huyo amesema kuwa halmashauri hiyo imejiwekea mradi wa kimkakati ili kuongeza mapato ya halmashauri ambapo wamepanga kujenga skimu ya umwagiliaji Katina bonde la Kisegese  ili kuboresha kilimo ambapo shilingi bilioni 13,195,356,140 zitatumika.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Innocent Mwangaza amesema bajeti hiyo inalenga kumsaidia mwananchi wa jimbo la Mlimba ambapo wameamua kuongeza vyanzo vipya vya mapato ikiwemo kukodisha majengo yao yaliyopo Ifakara na Mlimba na pia katika kujali afya za wananchi wameamua kuweka maduka ya madawa katika vituo vya Afya Mlimba na Lukolongo.

“Bajeti hii itamkomboa mwana Mlimba na msukumo wetu kama madiwani ni kuhakikisha mapato tunaweka mipango ya kuongeza mapato ikiwemo kukodisha majengo yetu tuliyoyaacha pale Ifakara na jengo la benki pale Mlimba na tumepanga kuyafikia maeneo yote wanayoishi wafugaji ili kujua wapo wangapi na mifugo ipo mingapi lengo ni kuwa na mifugo michache na kupata mapato halali,”alisema.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa