• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

Posted on: March 26th, 2025

Na; Milka Kaswamila- Afisa Habari Mlimba DC

Kamati ya Kudhibiti na Kukagua Shughuli za Serikali ( LAAC), tarehe 25.03.2025 imefanya ziara kwenye Halmashauri ya Wilaya Mlimba kukagua Mradi wa Ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi Mtendaji na Mradi wa Ujenzi wa Wodi Tatu na jengo la kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya, ya Halmashauri hiyo.

Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Halima Mdee ambapo awali walipokea taarifa ya miradi yote mitatu kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndg. Jamary Idrisa Abdul kisha wakauliza maswali na kuagiza Ofisi ya Mkurugenzi kuhakikisha Halmashauri inaendelea kufuata taratibu zote za upatikanaji wa vibali vya ujenzi wa miradi kutoka mamlaka za juu ikiwemo Ofisi ya Rais TAMISEMI na kutoa taarifa katika mamlaka zote husika endapo Halmashauri itafanya mabadiliko ya matumizi ya fedha za miradi.

Hata hivyo, kamati ya LAAC kupitia mwenyekiti wake, Mhe. Halima  Mdee wamesema  wameridhishwa na miradi waliyoikagua na wamempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo pamoja na timu yake ya wataalamu kwa usimamizi mzuri wakisema thamani ya fedha iliyo tumika imeendana na ubora wa majengo husika.

Kwa upande wake Naibu Waziri kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Festo Dugange amesema amependezwa kuona watumushi wa Halmashauri wakiwa na afya njema na miradi yao ikiwa ni mizuri.

“Tumeona nyumba ya Mkurugenzi nzuri sana, wodi za wagonjwa nzuri sana, Wakuu wa Idara ni wengi, watumishi wamenawiri,  na zaidi tumefurahi kuona mmeitumia vizuri nyongeza ya milioni 250 mliyoletewa na Ofisi ya TAMISEMI ili kukamilisha ujenzi wa zile wodi tatu. Hongereni sana”. Alisema Mhe. Dugange.

Kwa mujibu wa taarifa iliyo wasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji, Ndg. Jamary Idrisa Abdul, ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi umegharimu kiasi cha shilingi milioni 335.65 na wodi tatu na jengo la kuhifadhia maiti zimegharimu jumla ya shilingi milioni 971.37.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Wakili Dunstan Kyobya aliishukuru LAAC na kuahidi kuhakikisha anasimamia utekelezwaji makini wa maagizo yote iliyo yatoa kwa Halmashauri ya Mlimba. Aidha, alitumia wasaa huo kueleza mazuri ya Mlimba na kuwaalika wajumbe wa kamati kuwa mabalozi wa Mlimba kule waendako na wao kuja kuwekeza hasa katika sekta ya kilimo ambapo Halmashauri kwa sasa zao lake kubwa la biashara ni mchele, na mengine ni ufuta, kokoa, mbaazi, korosho na chikichi.

Hii ilikuwa ni ziara muhimu katika kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo inasimamiwa vyema na inawafaidisha wananchi wa Halmashauri ya Wilaya Mlimba.

Kamati ya LAAC inaendelea na kazi yake ya kudhibiti na kukagua shughuli za serikali ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Serikali za Mitaa unafanyika kwa usahihi na kwa manufaa ya umma.

MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA

    February 28, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI WA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA-MLIMBA

    February 08, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa