• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Madarasa 78 yaishe kwa wakati - DC Godigodi

Posted on: October 28th, 2021

MKUU wa wilaya ya Kilombero Hanji Godigodi ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Mlimba kuhakikisha kuwa inamaliza ujenzi wa vyumba vya madarasa 78 kabla ya Disemba 10 mwaka huu ili kujiandaa kuwapokea wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza mwakani.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kilichofanyika jana Mngeta wilayani humo,Godigodi amesema licha ya kukamilika kwa madarasa hayo pia yanatakiwa kukamilika madarasa shikizi mawili,nyumba moja ya mtumishi mtumishi na bweni moja la watoto.

Godigodi amesema halmashauri hiyo imepokea kiasi cha shilingi bilioni 1,680,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 78,bweni moja la watoto,nyumba moja ya mtumishi na madarasa mawili shikizi.

Amesema fedha hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuona wanafunzoi wote wanakaa madarasani na pia kuepusha wanafunzi hao na msongamano ambao unaweza kusababisha maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

Amebainisha kuwa licha ya kuwaepusha wanafunzi na ugonjwa wa Corona pia amewapunguzia wananchi katika uchangiaji wa ujenzi wa madarasa hivyo kuwataka wahusika kutumia vizuri fedha hizo na kutoa rai kuwa fedha hizo ni za moto na ataezichezea zitaondoka nae.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kwa juhudi za watendaji wa halmashauri na madiwani  ana uhakika wanafunzi wote waliofaulu wataingia darasani hapo Januari mwakani.

Amesema fedha zimeshaingia katika akaunti za shule hivyo kuiagiza menejimenti kuhakikisha kuwa kila diwani aliyepata fedha katika shule yake kujulishwa mapema ili nae aweze kuwajulisha wananchi wake anaowaongoza wafahamu fedha hizo zimetoka wapi.

Amewataka madiwani kusimamia fedha hizo ili kupata thamani ya fedha kwa ujenzi wa madarasa imara na madhubuti na wasiwaingilie mafundi katika kazi zao za utendaji.

Aidha mkuu huyo wa wilaya amewataka madiwani hao kuhamasisha wananchi wakapate chanjo ya Covid 19 kwani ni salama huku pia akiagiza wananchi wahimizwe na kwenda kwa watendaji kuchukua vitambulisho vyao vya uraia.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mlimba Innocent Mwangasa ameipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu kwa kuwapatia fedha hizo na kusema  kuwa zimefika kwa wakati na kuahidi kuwa watatekeleza maagizo ya mkuu wa wilaya ya kumaliza kwa wakati madarasa hayo.

Amesema ushirikiano  uliopo baina ya madiwani na watendaji katika halmashauri hiyo imekuwa chachu ya kukamilika kwa wakati kwa miradi mingi ya maendeleo na kuwaondolea wananchi kero mbalimbali hivyo kama serikali imeamua kuwasaidia wanaimani mambo mengi mazuri yanakuja katika halmashauri hiyo mpya.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Mhandisi Stephano Kaliwa amesema mpaka sasa wameshapokea fedha hizo na zimeelekezwa katika shule husika na kuahidi kuwa kuanzia sasa ujenzi utaanza mara moja na hakuna atakaekwamisha ujenzi huo.

Wilaya ya Kilombero imepokea zaidi ya shilingi bilioni 2.8 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba  133 vya madarasa ya sekondari,madarasa 22 ya shule shikizi,bweni moja la wanafunzi na nyumba moja ya mtumishi katika halmashauri mbili za Mlimba na mji Ifakara.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa