• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Mgomo wa wananchi kuhusu uwekaji mipaka kilombero waisha.

Posted on: October 25th, 2018

Pichani juu: baadhi ya wananchi wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya kilombero ndugu James Ihunyo, katika kikao cha maridhiano juu ya uwekaji wa mipaka katika vijiji vilivyopo jirani na pori tengefu wilayani humo.

Mkuu Wa Wilaya ya Kilombero kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya na viongozi Wa vyama vya siasa, wamemaliza mgomo uliokuwepo baina ya wananchi na wataalamu Wa wizara za Ardhi na Maliasili, kuhusu uwekaji upya wa mipaka katika vijiji 23 vilivyopo Jirani na pori tengefu wilayani humo.

Hivi karibu wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya makazi, kwa kushirikiana na wizara ya Maliasili na Utalii, waliamua kupitia na kuweka upya mipaka na hatimae kutengeneza ramani za vijiji, zinazotenganisha vijiji na eneo la pori tengefu la Kilombero katika Wilaya tatu za Kilombero,Ulanga na Malinyi.

Mpaka sasa, zoezi hilo limekwisha kamilika katika Wilaya Mbili za Ulanga na Malinyi, na lilitakiwa kuendelea katika Wilaya ya Kilombero lakini zoezi lilikwama baada ya wananchi kuligomea, kwa madai kuwa zoezi hilo halikuwa shirikishi na wataalamu walikuwa na lengo la kumega maeneo yao na hatimae wao kukosa maeneo ya makazi na shughuli za Kilimo.

Na baada ya msuguano huo ndipo timu ya kamati ya ulinzi na Usalama kwa kushirikisha viongozi Wa vyama vya siasa na wataalamu Wa wizara hizo Mbili waliamua kukutana na viongozi Wa kuanzia ngazi ya tarafa hadi vitongoji katika vijiji hivyo 23 ili kuzungumza nao na hatimae kufikia muafaka ili kufanikisha zoezi hilo.

Katika vikao vilivyofanyika katika tarafa Mbili za Mngeta na Mlimba viongozi hao walitoa kero zao na wataalamu kuwaelezea faida ya zoezi hilo hatimae muafaka ulipatikana na zoezi kuanza hivi karibuni.

Muafaka uliopatikana ni kwamba wataalamu hao watafika katika kila kijiji na kufanya mkutano na wananchi ili kuwaeleza faida ya zoezi na baadae kijiji kuteua watu 15 ambao watashirikiana na wataalamu hao kubaini mipaka ya kijiji na hatimae mipaka halali ikibainika itawekwa mipaka na hatimae kutengeneza ramani mpya.

Baada ya kuwekwa mipaka ambayo itakubaliwa na pande zote kitakachofuata ni wananchi kuheshimu mipaka hiyo na ni marufuku kwa wananchi kufanya shughuli za kibinadamu katika eneo LA pori tengefu.

Vijiji vilivyopo wilayani Kilombero ambavyo vitapitiwa na zoezi la kurekebisha mipaka yake ni Lumemo,Mahutanga,Miwangani,Namwawala,Idandu,Kalenga,Ikwambi,Mofu,Miomboni,Nakaguru na Ijia.

Vijiji vingine ni Isago,Luvilikila,Mkangawalo,Chita,Merera,Msita,Chisano,Kalangakelu,Msolwa,Mwembeni,Ipugusa na Ngalimila.

Hata hivyo habari njema ni kwamba kutokana na eneo kubwa la pori tengefu kuvamiwa na wananchi kuendeleza shughuli za kibinadamu serikali imeona ipunguze eneo hilo kutoka ukubwa Wa kilomita za mraba 6500 hadi kufikia kilomita 2900.

Mkuu Wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo amewataka wananchi kuwapa ushirikiano wataalamu hao ili zoezi likamilike kwa wakati na alama zikishawekwa wananchi waelewe maeneo yao halali ili kujiandaa na msimu mpya Wa Kilimo.

Ikumbukwe kuwa eneo la pori tengefu la Kilombero, ndio Chanzo cha uzalishaji Mkubwa Wa Maji katika Mto Kilombero, ambayo ndio tegemeo la uzalishaji Mkubwa Wa umeme katika maporomoko ya Mto Rufiji, na pia katika eneo la pori tengefu ndipo lipo eneo la Ardhi chepechepe (Ramsar).

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa