• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

SPIKA TULIA ASAIDIA WAHITAJI CHING'ANDA MLIMBA

Posted on: July 26th, 2024

Na, Milka Kaswamila- Mlimba DC

Mwenyekiti wa Taasisi ya Tulia Trust Fund, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani mhe. Dkt. Tulia Akson, leo tarehe 26.07.2024 amekabidhi nyumba kwa mwananchi wa kijiji cha Chin’ganda Kata ya Chita, aliyekuwa akiishi kwenye mazingira hatarishi yeye pamoja na familia yake.

Wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara, kabla kukabidhi nyumba hiyo, mhe. Tulia amesema Taasisi yake inatoa misaada ya namna hiyo ili kuwapa hamasa watanzania wenye uwezo waone umuhimu wa kuwasaidia watu ambao hakika wanayo mahitaji.

“Sisi tumeamua kutoa msaada kwa kuongea sio kimya kimya ili watanzania wenzetu ambao Mungu amewajalia uwezo, wahamasike na wao kutoa misaada kwa wahitaji walio katika maeneo yao na hata nje ya maeneo yao” alieleza Dkt. Tulia.

Pia, Dkt. Tulia alitumia nafasi hiyo kuwaeleza wananchi mambo mazuri ambayo Rais Samia ameyafanya katika Halmashauri ya Mlimba, ikiwemo kuridhia ujenzi wa barabara ya lami toka Lumemo Ifakara hadi Chita JKT Mlimba, upatikanaji wa huduma za maji na umeme na ujenzi wa shule, vituo vya afya na Hospitali ya Wilaya.

Hata hivyo, Dkt. Tulia amepokea kilio cha wananchi wa Chin’ganda, ambacho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlimba mhe. Innocent Mwangasa na Mbunge wa jimbo la Mlimba mhe. Godwin Kunambi amekiwasilisha kwake kumsihi Rais Samia ujenzi wa barabara hiyo ya Lumemo- Chita uanze.

Naye mwananchi aliyejengewa nyumba, amemshukuru sana Dkt. Tulia kwa moyo wake wa upendo na amemuombea baraka katika utekelezaji wa majukumu yake na maisha yake kwa ujumla.

Kwa mujibu wa msemaji wa Tulia Trust Fund, nyumba hii iliyojengwa Chin’ganda ni ya 14 ambapo nyumba zingine zimejengwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo mkoa wa Mbeya.

Aidha, ujio huu wa Dkt. Tulia umekuwa neema kwa mtoto mwenye mahitaji maalumu na Jeshi la polisi Wilaya ya Kilombero kwa sababu ametoa msaada wa kiti mwendo kwa mtoto huyo na boksi 45 za vigae (Tiles) kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la Ofisi ya polisi kwenye kijiji cha Chin’ganda.

MWISHO


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa