• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOMBERO YAZINDUA JUKWAA LA WANAWAKE LA KUWEZESHWA KIUCHUMI

Posted on: April 29th, 2017

Katibu tawala wa wilaya ya Kilombero Mh. Robert Selasela amezindua rasmi jukwaa la wanawake la uwezeshwaji kiuchumi la halmashauri ya wilaya ya Kilombero. Akihutubia katika kilele cha uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa Mount - peak katika tarafa ya Mang'ula kata ya Mwaya Selasela amewaambia wanawake wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero kwamba uzinduzi wa jukwaa la wanawake ni agizo la Mheshimiwa makamu wa rais wa jamhururi ya muungano wa Tanzania Mh. Samia  Salum ambapo alitaka kila wilaya iunde jukwaa la kiuchumi la  uwezeshaji wanawake na baadaye jukwaa hilo liundwe pia kwa ngazi ya kila kata.


Mh Selasela ametanabaisha kuwa lengo la serikali ni kutoa fursa kwa wanawake kujisimamia wenyewe kwa kushirikiana na serikali kupitia fursa zilizopo za uzalishaji, masoko, uwekezaji na za kiuchumi ili waweze kuchochea maendeleo wao wenyewe. Awali katika dua ya ufunguzi wa hafla ya uzinduzi Viongozi wa dini waliwasisitiza wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi kutumia fursa zao bila kukiuka misingi ya dini kwa wanawake kuwaheshimu waume zao na wanaume kuwathamini wake zao ili kila mtu atimilize wajibu wake katika shughuli za kila siku.

Aidha katibu tawala amesisitiza umuhimu wa jukwaa la uwezeshaji ni pamoja na kutaka kubadirisha fikra za watu kwa kuleta ukombozi wa kweli kwa kuanza na uchumi, Mh selasela ameongeza kwa kusema kukiwa na uchumi mzuri wanawake watasoma vizuri, watapata huduma bora ya afya na kuimarisha huduma ya mama na mtoto kupitia vituo vya afya.


Ofisi ya mkuu wa wilaya kupitia uzinduzi wa baraza la wanawake la halmashauri ya wilaya ya Kilombero imeiagiza ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero kuhakikisha mpaka ifikapo tarehe 30.05.2017 kila kata iwe imekwishafanya uchaguzi wa viongozi wa jukwaa la wanawake uwezeshwaji kiuchumi katika ngazi ya kata na kutoa ripoti ya uchaguzi huo katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kilombero, na ifikapo tarehe 30.06.2017 kikao cha kwanza cha viongozi wa ngazi ya wilaya na viongozi wa kila kata kiwe kimeshafanyika ili mwenyekiti wa Halmashauri, mwenyekiti wa jukwaa la wanawake na makamu mwenyekiti waweze kuwaeleza viongozi waliochaguiwa majukumu yao ili azima ya kuwachagua na kuwapa majukumu itekelezwa na wawe tayali kwa kuanza kazi, Mh selasela amemalizia kwa kusisitiza kwamba baraza la wanawake kwa ngazi ya kata ndilo litakalokuwa na majukumu ya kutambua vikundi vya wanawake vyenye stahili ya kukopesheka.


Uzinduzi wa baraza la wanawake umefanikiwa kupata viongozi mbalimbali waliochaguliwa katika nafasi mbalimbali, Bi. Amina Rashid Mrisho amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Kilombero huku Bi. Zafimara Hassani Kuhuka akiibuka kuwa makamu mwenyekiti, wengine waliochaguliwa ni pamoja na Bi. Lucy Charles Msisia ambaye yeye anakuwa katibu wa jukwaa la wanawake la kuwezeshwa kiuchumi na Bi. Consolalya Liampawe ambaye ni Mhazini wa jukwaa kwa ngazi ya Halmashauri ya wilaya ya Kilombero.


Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI JAMARY AWAPOKEA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

    June 10, 2025
  • MHE. WAZIRI WA MAMBO YA NJE KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MLIMBA DC

    June 04, 2025
  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa