• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MLIMBA DISTRICT COUNCIL
MLIMBA DISTRICT COUNCIL

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko/ Asili
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
      • Muonekano wa muundo
    • Idara/ Vitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Miundombinu
      • Fedha na Biashara
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango, Takwimu na ushirika
      • Mazingira na Usafi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi, Maliasili na Mazingira
      • Ufugaji na uvuvi
      • CHF iliyoboreshwa
      • Sheria
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za watumishi
    • Rasilimali watu
    • TEHAMA
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha, utawala na mipango
      • Elimu, Afya na maji
      • Uchumi, Ujenzi na mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa madiwani
      • Kumuona mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
      • PICHA ZA MIRADI YA MAPAMBANO DHINI YA UVICO

Waziri Ulega amaliza kero za wananchi wa miwangani dhidi ya RAMSAR

Posted on: December 12th, 2018

Pichani juu: Mfugaji akisoma Risala kwaajili ya wafugaji wenzie mbele ya Naibu waziri wa mifugo na Uvuvi

Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi Abdalah Ulega amekutana na wananchi wa Kijiji cha Miwangani Kata ya Idete Wilayani Kilombero, ili kutatua mgogogro uliokuwepo baina ya Maliasili ya Hifadhi ya pori tengefu (RAMSAR), pamoja na wafugaji wa kijiji hicho ambao wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kilimo, ufugaji pamoja na uvuvi.

Hiyo ikiwa ni Ziara yake ya kwanza katika kijiji hicho, ambapo wananchi waliweza kueleza matatizo yao huku wakiinyooshea vidole Maliasili (RAMSAR) kuwa ndiyo wasababishaji wakubwa wa matatizo yanayotokea kijini hapo na hasa katika mgogoro wa wakulima na wafugaji kwa kuingiliana baadhi ya maeneo yao.

Kwa upande wa wafugaji wameeleza malalamiko yao kuwa wanateseka kwa kukosa sehemu za marisho kwaajili ya mifugo yao, na hii ni  kutokana na kuingiliwa na wakulima katika maeneo yao, kuzuiliwa mifugo yao kwenda katika mto kwa ajili ya  kunywa maji, pia baadhi ya maeneo yao kuchukuliwa na RAMSAR.

AIidha baadhi ya wafugaji kutoka katika kijiji cha Mchombe Wilayani humo, wameomba kuachiwa birika la kunywea maji mifugo ambalo awali walikuwa wakilitumia ila kwa sasa liko chini ya Hifadhiya pori tengefu (RAMSAR) kwa madai ya kwamba limejengwa ndani ya eneo lao, hivyo kwa sasa hawana  sehemu ya kunyweshea maji mifugo yao ukizingatia mifugo ni uharibifu wa vyanzo vya maji.

Pia wakulima nao wameeleza malalamiko yao kwa wafugaji ambao wanaruhusu mifugo yao kuingia katika mashamba yao na kupelekea uharibifu wa mazao bila ya kujali kuwa wao ni wageni katika eneo hilo na badala yake kujifanya wao ndiyo watawala  wa kijiji hicho cha miwangani.

Lakini pia kwa upande wa wavuvi  nao wameeleza kero yao kwa kuwaelekezea RAMSAR , na hii ni kutokana na eneo la maji  kuchukuliwa na RAMSAR ambapo hawajui nini hatima ya shughuli zao za uvuvi ukizingatia wengine tayari wana leseni.

Hata hivyo kutokana na matatizo yaliyomesemwa na wanakijiji wa miwangani kuonekana yanasababishwa na RAMSAR , Kaimu meneja wa Maliasili  na hifadhi ya pori tengefu, aliweza kujibu hoja zao kwa kusema kuwa kwa kawaida kijiji cha miwangani chote kipo ndani ya hifadhi ya pori tengefu, hivyo hata kwa baadhi ya maeneo ambayo wako nayo wanakiji kwa sasa hivi, RAMSAR imeamua kuwaachia tu kama kuwahurumia kutokana na baadhi ya maeneo tayali yamekuwa na huduma za kijamii kama vile makazi, shule na vituo vya afya, wameamua kuwaachia hivyo hawawezi kuwaamuru wavibomoe.

Sanjari na hayo Mheshimiwa Ulega amejibu hoja za wanakijiji hao kuwa  mpaka sasa sheria haijakataza shughuli za uvuvi, isipokuwa serikali imetaka wavuvi wajisajili katika vikundi vya uvuvi halali ili wasisumbuke na waweze kuwa huru, na wakati huo huo kutoa muda wa mwezi mmoja kwa viongozi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero kuwakatisha leseni na kuwasajiri wavuvi hao na kutoa wito kwa Ramsa kuwa wawe wanatumia maarifa pindi wanapotaka kuyachukua maeneo yao kwa kuwatimizia baadhi ya vitu, kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kusaidia kuepusha baadhi ya migogoro katika jamii.

Zaidi ya hayo halmashauri imetakiwa kujenga Maramba matano kwaajili ya kuwasaidia wavuvi hao

Matangazo

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MWANDIKISHAJI MSAIDIZI NA MWENDESHAJI WA VIFAA VYA BAYOMETRIKI February 13, 2025
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWEZI DESEMBA 2024 January 07, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) YA MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI MWAKA 2024 January 05, 2025
  • KIUNGANISHI (LINK) CHA MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA UPIMAJI WA DARASA LA NNE MWAKA 2024 January 05, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MLIMBA DC YAPOKEA VITABU 13,607 KWA AJILI YA SHULE ZAKE ZA SEKONDARI

    May 30, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA VIFAA VYA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 29, 2025
  • TUME HURU YA UCHAGUZI YATANGAZA MAJIMBO MAPYA

    May 31, 2025
  • LAAC YAKAGUA MIRADI MLIMBA DC

    March 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Kupata Madarakani au cheo hakukufanyi kujua kila kitu. Maneno ya hekima kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu Mhe. Mhe. Dkt Doto Biteko
video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Fomu ya maombi ya ruhusa
  • Fomu ya utambulisho benki
  • Fomu ya Kuhuisha Uanachama CHF iliyoboreshwa
  • Wasifu wa Wilaya
  • Muundo wa Halmashauri
  • Eneo la Kijiografia
  • Fursa za Uwekezaji Kilombero

Viunganishi linganifu

  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ikulu
  • Idara kuu ya Takwimu (NBS)
  • TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

kitafutio cha watembeleaji wa duniani

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Mngeta Kijiji cha Itongoa

    Anuani: P.O.BOX 263

    Simu: 023 293 1523

    Mobile: 0232931523

    Barua pepe: ded@kilomberodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.Haki zote zimehifadhiwa